Wednesday, February 22, 2012

ZAFEPED yatakiwa kubuni mbinu mbadala za kuwasaidia wananchi kutokana na umasikini

Na Is-haka Omar ZPC Zanzibar
Mkuu wa wilaya ya kusini Bw Haji Makungu Mgongo amewataka wanajumuiya ya kupambana na umasikini na uharibifu wa mazingira ZAFAPED kubuni mbinu mbali mbali zitakazowasaidia wananchi kuondokana na umasikini .
Akizungumza na viongozi wa jumuiya hiyo ofisini kwake amesema wananchi wengi wa wilaya ya kusini wanatengemea misitu katika kupata ajira hali inayosababisha uharibifu mkubwa wa mazingira .
Amesema ili wananchi waondokane na tatizo la uharibifu wa mazingira ipo haj ya kutoa elimu kuondokana na uharibifu wa mazingira ikiwemo misitu katika wilaya hiyo tatizo ambalo limedumu kwa muda mrefu .
Nae Mkurungezi wa jumuiya hiyo Bw. Faida Khamisi Ali amesema lengo kuu la jumuiya hiyo ni kuwapatia wananchi elimu na mbinu za kupambana na umasikini .
Jumuiya hiyo inafanya kazi zanzibar katika shehia za wilaya ya kusini ikiwemo mtende ,pete na kajegwa kwa kupitia mradi wa hima na Care tanzania ambapo mradi huo utakuwa wa mienzi sita .

No comments:

Post a Comment