Friday, February 24, 2012

Waandishi watakiwa wawe wafuatailiaji wa kina juu ya matukio na masuala yawahusuo watu wenye kuishi na ulemavu

Na Is-haka Omar ZPC
Waandishi wa habari nchini wametakiwa kushiriki kikamilifu katika kufuatilia kwa kina na kuandika habari na matukio mbalimbali ya watu wenye ulemavu ili waweze kupata haki zao za msingi kisheria.
hayo yameelezwa na mwenyekiti wa bodi kutoka ofisi ya umoja wa watu wenye ulemavu Zanzibar Bw.Ali Omar Makame wakati akifungua mafunzo ya siku 3 huko katika ukumbi wa jumuiya hiyo weres kwa waandishi wa habari juu ya kutambua haki za msingi za watu wenye ulemavu kisheria.
Amesema waandishi wa habari watumie taaluma yao katika kuelimisha jamii kwa kuandika habari na kufichua maovu wanayofanyiwa watu wenye ulemavu ili nao wapate haki zao za msingi kama watu wengine katika jamii.
Aidha Bw.mMakame amefahamisha kuwa watu wenye ulemavu wanatakiwa kushirikishwa katika mambo mbalimbali yanayowahusu hususani kijamii,kiuchumi na kisiasa.
Nae mwezeshaji katika mafunzo hayo bw.ali saleh amesema watu wenye ulemavu katika mkataba wa kimataifa wanatakiwa kuwa na fursa iliyo sawa kwa manufaa ya taifa katika nyanja zote za kijamii na katika hali yoyote inayojumuisha upatikanaji wa elimu, habari, mawasiliano na mazingira ya kimaumbile.
Bw.Saleh amesema kuwa sheria namba 9 ya mwaka 2006 ya Zanzibar ya watu wenye ulemavu inamapungufu katika suala zima la utekerezwaji kwani walengwa wa sheria hiyo hawapatiwi haki zao kwa mujibu wa sheria inavyoeleza hususani katika ujenzi wa majengo ya serikali pamoja na asasi za kiraia hawazingatii miundo mbinu inayoendana na mazingira halisi ya watu wenye ulemavu na kusababisha usumbufu mkubwa bindi wanapotaka kupata huduma mbalimbali za kijamii.

No comments:

Post a Comment