Saturday, February 25, 2012

Kampeni ya maliza malaria yapamba moto Zanzibar

Na Is-haka Omar ZPC
Kitengo cha kupambana na malaria Zanzibar kimeanza kazi za usajili wa kaya ikiwa ni matayarisho ya ugawaji wa vyandarua unaotarajiwa kufanyika mapema mwezi ujao.
Kazi hizo zilizoanza jana zitaendelea kwa muda wa siku tatu ili kupata idadi sahihi ya kaya zitakazopatiwa vyandarua ambapo kwa mujibu wa kitengo hicho kiasi vyandarua laki saba vitagaiwa bure kwa wananchi wa Unguja na Pemba..
Meneja wa kitengo cha kupambana na malaria Bw.Abdalla Suleiman amesema kiasi ya vijana elfu mbili wa wilaya zote wamepatiwa mafunzo ya usajili wa kaya na kusambaza vyandarua kwa wananchi.
Amefahamisha hatua hiyo itasaidia kufanikisha ugawaji wa vyandarua na kutoa wito kwa wananchi kutodharau usajili huo ili kila kaya ipate chandarua kwa lengo la kutomeza malaria Zanzibar.

No comments:

Post a Comment