Saturday, February 25, 2012

Mkuu wa Mkoa wa mjini azuwiya ujenzi katika wilaya yake

Na Is-haka Omar ZPC
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Bw.Abadalla Mwinyi Khamis ametoa agizo la kuzia uuzaji wa viwanja na ujenzi wa aina yoyote katika eneo ambalo wananchi wa shehia ya mbuzini wanalihitaji kulitumia kwa ujenzi wa miradi ya kijamii.
Amesema tabia inayofanywa na baadhi ya watu kuuziana viwanja kiholela si utaratibu unaofaa hivyo ameuagiza uongozi wa wilaya ya Magharibi kushirikiana na wananchi wa eneo hilo kuliomba eneo hilo kwa wizara ya ardhi ili kupata umiliki na kulitumia kwa malengo yao.
Ametoa agizo hilo wakati wa ziara huko mbuzini kufuatia malalamiko ya wananchi kuhusu kuwepo kwa baadhi ya viongozi kuuza viwanja kwenye neo hilo.
Nao wananchi wa Mbuzini wameelezea kusikitishwa na vitendo vinavyofanywa na baadhi ya viongozi kuuza viwanja ovyo pamoja na kuutupia lawama uongozi wa jimbo kwa kushindwa kufuatilia suala hilo.
Wakati huo huo mkuu huyo wa mkoa amefanya ziara shehia ya Fuoni Pangawe kuona uharibifu wa mazingira unaofanywa kwa uchimbaji mchanga na kuutaka uongozi wa shehia hiyo kuimarisha polisi shirikishi jamii ili walinde maeneo yao.

No comments:

Post a Comment