Friday, February 24, 2012

Serikali yatakiwa kulipatia ufumbuzi tatizo la ubovu wa barabara ya Kinuni-Unguja

Na Is-haka Omar ZPC
Wananchi wa shehia ya Kinuni wameiomba serikali kuwatatulia tatizo la ubovu wa barabara ya eneo hilo ili kuwaepushia usumbufu wanaopata.
Wamesema wakati umefika kwa serikali na taasisi binafsi kuweka mikakati mbalimbali ili kuona barabara za maeneo mbalimbali ikiwemo ya eneo hilo zinajengwa na kuimarishwa kwa lengo la kuwaondolea wananchi usumbufu katika utekelezaji wa shughuli zao za kila siku.
Wakizungumza na waandishi wa habari hizi wamesema wamekuwa wakikabiliwa na usumbufu mkubwa pale wanapokuwa safarini kutokana na ubovu wa barabara hiyo jambo ambalo linawaresha nyuma maendeleo yao.
Hivyo wamesema kukosekana kwa barabara ya uhakiki katika shehia hiyo kunasababisha kutofanyika shughuli zao kwa ufanisi zaidi

No comments:

Post a Comment