Wednesday, November 14, 2012

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Dodoma



SMZ: Yasisitiza afya ya uzazi wa pango

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema kuwa jamii inahitaji kuelimishwa zaidi juu ya umuhimu wa uzazi wa mpango kwa maendeleo ya nchi na kutunza afya ya jamii hasa kwa akina mama na watoto.

Kauli hiyo imetolewa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad katika hafla ya uzinduzi wa Ripoti ya Idadi ya Watu Duniani ya mwaka 2012 iliyofanyika katika viwanja vya skuli ya Mkwajuni Mkoa wa Kaskazini Unguja, ambako alimuwakilisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohd Shein.

Amesema jamii bado haijatoa umuhimu unaostahiki katika matumizi ya njia za uzazi wa mpango, hali inayopelekea kuwepo kwa ongezeko kubwa la watu ambalo huathiri harakati za maendeleo na afya ya jamii.

“Taarifa zinaonesha kwamba Zanzibar hivi sasa inakadiriwa kuwa na idadi ya watu 1.3 milioni, wanaoongezeka kwa kasi ya asilimia 3.1 kwa mwaka ambapo idadi ya watu katika kila kilomita moja ya mraba imefikia watu 496 mwaka 2011”, ilieleza sehemu ya hotuba hiyo ya Dkt. Shein iliyosomwa na Makamu wa Kwanza wa Rais.

Amefahamisha kuwa bado vifo vya mama wajawazito viko juu duniani lakini vimepungua kwa upande wa Tanzania na Zanzibar hasa kwa kina mama wenye umri mdogo na wanaokabiliwa na tatizo la umaskini.

“Kwa Tanzania katika mwaka 2004/05 idadi ya vifo ilikuwa 578 kwa kila akina mama waja wazito 100,000 na kupungua kidogo hadi kufikia vifo 454 mwaka 2010. Hata hivyo kwa Zanzibar vifo vya akina mama vimepungua kutoka vifo 473 mwaka 2006 hadi vifo 281 mwaka 2011, kwa kila kina mama 100,000 kwa takwimu za hospitali”, alifafanua.

Amesema mafanikio hayo yametokana na juhudi za serikali katika kuimarisha huduma za afya kwa jamii ikiwa ni pamoja na kutoa chanjo za pepopunda na shurua, sambamba na kuimarisha huduma za afya ya uzazi katika hospitali mbali mbali.

Kwa upande wao wawakilishi wa Umoja wa Mataifa wameipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuona umuhimu wa huduma ya uzazi na kuamua kutoa huduma hiyo bila ya malipo.

Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Idadi ya watu (UNFPA) Tanzania bibi Mariam Khan amesema bado suala la uzazi wa mpango linakabiliwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na wanajamii kuona ugumu juu ya matumizi ya njia za uzazi wa mpango.

Amefahamisha kuwa uzazi wa mpango ni muhimu katika kusaidia kukuza kipato cha wanafamilia, sambamba na kuwaendeleza watoto katika makuzi bora, na wito kwa jamii kutoa fursa zinazostahiki kwa akina mama na watoto ili kusaidia harakati za maendeleo kwa jamii.

Waziri wa Afya Mhe. Juma Duni Haji amesema wameamua kufanya uzinduzi huo katika Mkoa wa Kaskazini Unguja, ili kutoa uelewa zaidi kwa wakaazi wa Mkoa huo ambao ni miongoni mwa mikoa inayofanya vibaya katika suala la uzazi wa mpango.

Amesema akinamama na watoto wanahitaji kulindwa kiafya, na kuwataka wazazi kushirikiana katika suala la malezi na makuzi ya watoto.

Mapema akitoa muhtasari wa ripoti hiyo, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo Khamis Mussa amesema kimsingi ripoti hiyo imeelezea juu ya changamoto, faida na haki za binadamu katika uzazi wa mpango.

Amesema uzazi wa mpango ni miongoni kwa haki za binadamu lakini imeelekezwa zaidi kwenye haki za kifamilia, ili wanafamilia waweze kupanga juu ya idadi na umri wa kupishana kwa watoto, ili kuepuka mimba zisizotarajiwa.

“Inakisiwa kuwa kiasi cha mimba milioni 80 zinapatikana bila ya kutarajiwa duniani, huku nusu ya mimba hizo zikitolewa, jambo ambalo ni hatari nyengine katika uzazi”. Alidokeza Katibu Mkuu huyo.

Hassan Hamad, OMKR.

Friday, November 9, 2012

Dr.Shein ampongeza Obama

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein ametuma salamu za pongezi kufuatia ushindi wa Rais Barack Obama wa Marekani katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo uliofanyika hivi karibuni.
 
Katika salamu zake za pongezi kwa kiongozi huyo wa Marekani ambaye amechaguliwa kwa mara nyengine tena na wananchi wa nchi hiyo kwa kipindi cha pili, Rais Dk. Shein alieleza jinsi alivyopokea kwa furaha ushindi huo pamoja na wananchi wote wa Zanzibar.
 
Salamu hizo za pongezi zilieleza kuwa kwa niaba yake binafsi pamoja na wananchi wa Zanzibar anatuma salamu za pongezi kwa Rais Obama kwa ushindi mkubwa alioupata katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni nchini humo.
 
Aidha, salamu hizo zilieleza kuwa  wananchi wa Marekani wameona umuhimu wa kumuunga mkono Rais Obama na kumrejesha tena madarakani kwa lengo la kuliendeleza na kuliongoza taifa hilo kubwa duniani kwa kipindi cha miaka mine ijayo.
 
Pamoja na hayo, salamu hizo zilieleza kuwa wananchi wa Zanzibar wanaungana na rafiki zao wa Marekani katika kusherehekea ushindi huo uliotokana na uchaguzi mkuu wa hivi karibuni wa Marekani ambao umempa ushindi Rais Obama.
 
Dk. Shein alimtakia uongozi mwema Rais Obama na kutoa salamu za pongezi kwa familia ya Rais Obama akiwemo Mkewe Mama Michelle Obama  na watoto wake wote Malia na Sasha Obama  pamoja na wananchi  wa Marekani ambao wameonesha wazi imani na uaminifu mkubwa walionao katika uongozi wa Rais Obama.
 
Sambamba na hayo, salamu hizo zilieleza kuwa  uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya Zanzibar na Marekani utazidi kuimarika.
 
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar.

Balozi wa India akutana na Dr.Shein Ikulu Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameleza haja kwa Serikali ya India kurejesha utamaduni uliokuwa ukifanya miaka ya nyuma wa kuwaleta madaktari bigwa kwa amu hapa Zanzibar hatua ambayo ilisadia sana kuimarisha sekta ya afya na kutoa huduma kwa jamii wakati huo.

Dk. Shein aliyasema hayo leo wakati alipokuwa na mazungumzo na Balozi mdogo wa India aliopo Zanzibar Mhe. Pawan Kumar ambaye alifika Ikulu mjini Zanzibar kwa ajili ya kujitambulisha.


Dk. Shein alisema kuwa mnamo miaka ya 1970 hadi mwanzoni mwa miaka ya 1980, India ilikuwa na utaratibu huo wa kutela madaktari bingwa hapa Zanzibar ambao waliweza kufanya kazi zao na kutoa huduma za afya kwa wananchi hatua ambayo ni busara kuanzishwa tena ili kuendeleza kuimarisha sekta ya afya hapa Zanzibar.


Katika maelezo yake Dk. Shein alisema kuwa kuwepo kwa madaktari bigwa hapa nchini kutoka India kutasaida zaidi kuimarisha huduma katika hospitali za Zanzibar hasa hospitali za Wete na Chake kisiwani Pemba ambazo kwa hivi sasa zina upungufu wa madaktari bigwa.


Mbali na hatua hiyo, Dk. Shein alisisitiza umuhimu wa kubadilishana uzoefu na utaalamu kwa madatari wa India na Zanzibar kwa awamu, juhudi ambazo zitasaidia kuipinguzia gharama Serikali ya kupelekea wagonjwa katika hospitali zilizopo nchini humo.
 
Aidha, Dk. Shein alieleza haja ya kuanzisha Mkataba wa Makubaliano juu ya kuimarisha sekta ya afya kati ya India na Zanzibar.

Pia Dk. Shein alimueleza Balozi huyo uhusiano wa siku nyingi katika sanaa ya uimbaji ambao upo kati ya India na Zanzibar hali ambayo ilimpelekea mwimbaji maarufu marehemu Siti Binti Saad kwenda kurikodi katika studio za nchi hiyo nyimbo zake mbali mbali ambazo zilimjengea sifa kubwa duniani.


Kwa upande wa sekta ya kilimo, Dk. Shein alieleza kuwa kutokana na India na Zanzibar kufanana kijiografia kuna umuhimu wa nchi hizo kuendeleza ushirikiano katika sekta hiyo ambayo ni tegemeo kubwa la uchumi wa Zanzibar na wananchi wenyewe.


Dk. Shein alieleza kuwa India ni miongoni mwa nchi zilizopiga hatua katika kufanya utafiti wa kilimo hivyo alieleza haja ya kuimarisha ushirikiano katika sekta hiyo hasa kwa kushirikiana na wataalamu wa Kitengo cha Utafiti wa Kilimo kiliopo Kizimbani.


Kutokana na Balozi huyo kuwa mpya katika mazingira ya Zanzibar Dk. Shein alimshauri kutembelea katika maeneo ya kilimo cha mpunga ili aweze kuona uhalisia na hatua zilizofikiwa na wananchi pamoja na juhudi za serikali za uimarishaji wa sekta hiyo.


Akieleza juu ya zao la karafuu, Dk. Shein alimueleza Balozi huyo kuwa kwa vile India wana historia ya ununuzi na utumiaji wa karafuu kutoka Zanzibar hivyo ipo haja kya kuimarisha ushirikiano wa kibiashara katika zao hilo.


Pia, Dk. Shein alipongeza maendeleo makubwa yaliofikiwa na India katika sekta ya elimu na kueleza kuwa nchi hiyo hivi sasa imekuwa ikitoa mafunzo mbali mbali kwa wanafunzi kutoka nchi tofauti duniani na kueleza kufarajika kwake kutokana na wanafunzi wengi wanaotoka Zanzibar na kwenda nchini humo kusoma fani mbali mbali.


Sambamba na hayo, Dk. Shein alisisitiza haja ya kuendeleza ushirikiano katika sekta hiyo ya elimu huku akipongeza juhudi za India za kutaka kuanzisha Chuo cha Mafunzo ya Amali huko kisiwani Pemba pamoja na juhudi za kuanzisha mradi wa kutoa mafunzo kwa watoto wa kike vijijini.


Nae Balozi huyo mdogo wa India aliopo hapa Zanzibar Mhe. Pawan Kumar alimueleza Dk. Shein kuwa nchi yake itaendeleza uhusiano na ushirikiano uliopo ambao ni wa muda mrefu na umekuwa na historia kubwa.


Balozi Pawan Kumar alieleza kupokea rai zilizotolewa na Dk. Shein katika kuimarisha sekta ya afya nchini pamoja kuahidi kuzifanyia kazi ipasavyo.


Alieleza kuwa kwa upande wa sekta ya Afya India itaendelea kuiunga mkono Zanzibar katika sekta hiyo ikiwa ni pamoja na kuendelea kutoa nafasi za masomo kwa madaktari wazalendo. Aidha, Balozi huyo alieleza kuwa mbali ya nafasi za masomo kwa madaktari wazalendo pia, nchi hiyo itaendelea kutoa nafasi za masomo katika fani nyengine tofauti.
 

Balozi Pawan Kumar pia, alibainisha kuendeleza ushirikiano katika kuimarisha nishati pamoja na juhudi za kujikinga na maafa.

Pamoja na hayo, Balozi huyo alimueleza Dk. Shein azma ya India ya kujenga Chuo cha Amali kisiwani Pemba, hatua ambayo itasaidia katika kuimarisha sekta ya ajira na kutoa utaalamu kwa wananchi.
 

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar.

Wednesday, October 17, 2012

Dk.Shein awaapisha viongozi wapya

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha viongozi na watendaji katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kufuatia uteuzi alioufanya hivi karibuni.
 
Katika hafla hiyo iliyofanyika Ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali Dk. Shein alimuapisha Mhe. Shawana Bukheti Hassan ambaye ameapishwa kuwa  Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri asiekuwa na Wizara Maalum.
 
Miongoni mwa viongozi waliohudhuria ni Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Pili wa Rais Mhe. Balozi Seif Ali Idd, Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Pandu Ameir Kificho, Waziri wa Nchi Afisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Mwinyihaji Makame
 
Wengine ni Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe. Mohammed Aboud, Waziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati Mhe. Ramadhan Abdalla Shaaban, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdillahi Jihad Hassan, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Abdalla Mwinyi Khamis, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar, Mstahiki Khatib Abdulrahman Khatib pamoja na viongozi wengine.
 
Wakati huo huo, Dk. Shein amewaapisha viongozi wengine akiwemo Naibu Waziri wa Kilimo na Maliasili Mhe. Mtumwa Kheir Mbarak pamoja na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mohamed Said Mohamed.
 
Viongozi wengine walioapishwa katika hafla hiyo ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano Bwana Tahir M. Abdalla pamoja na Bwana Mustafa Aboud Jumbe ambaye ambae ameapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano.
 
Pia, Dk. Shein amemuapisha Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi anaeshughulikia Idara Maalum za SMZ, CDR Julius Nalimy Maziku pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais (Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo) Bwana Juma Ameir Hafidh.
 
Hapo juzi, Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein alifanya mabadiliko ya viongozi na watendaji wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kutumia uwezo aliopewa chini ya vifungu vya  Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ambapo pia, alifuta rasmi uteuzi wa Mhe. Mansoor Yussuf Himid kuwa Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi kuanzia Oktoba 15 mwaka huu na Mhe. Shawana Bukheti Hassan aliteuliwa kuwa Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi.
Rajab Mkasaba, Ikulu

Tuesday, September 11, 2012

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


KUUAWA KWA MWENYEKITI WA KLABU YA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA IRINGA (IPC) DAUDI MWANGOSI 
 Zanzibar Press Club imepokea kwa masikitiko na hudhuni  taarifa ya kifo cha mwandishi wa habari wa kituo cha Channel Ten ambaye pia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari wa Iringa.  
Zanzibar Press Club inaungana na waandishi wa habari wote nchini ambao leo hii wanatekeleza azimio la jukwaa la Wahariri la kufanya maandamo ya kimya kimya, kote nchini, kwa lengo la kupinga mauwaji ya aliyekuwa Mwenyekiti Klabu ya waandishi wa habari wa Iringa, Mrehemu Daudi Mwangosi.
Katika kutekeleza azimio hilo ZPC imeamuwa kukutana na waandishi wa habari ili kuweza kueleza kusikitishwa kwao na tukio hilo lilompata mwenzetu wakati akitekeleza majukumu yake ya kila siku.
Aidha ZPC inaungana na waandishi na wafanyakazi katika tasnia ya habari nchini, Umoja wa Waandishi wa Habari nchini (UTPC), Klabu za waandishi kote nchini, MISA-TAN, MCT, JUKWAA LA WAHARIRI  n.k  pamoja na familia ya marehemu Daudi Mwangosi kwenye kipindi  hiki kigumu cha msiba, ambapo hakuna shaka kwamba tasnia ya habari nchini imelazimika kuingia matatani kutokana na matumizi mabaya ya nguvu na  mabavu ya Jeshi la Polisi.
ZPC inalaani kwa nguvu zote mauwaji hayo na yaliyofanywa na watendaji wa taasisi ya umma pamoja na kutumia nguvu nyingi kupiti kiasi zilizopelekea kifo cha mwandishi huyo.
Jeshi la Polisi limekuwa likiendeleza tabia yake ya  matumizi ya nguvu kupita kiasi kwa raia wa taifa hili. Ipo haya ya kutaka kujuwa ni hadi lini jeshi la polisi wataweza kuimarisha vyema shughuli za ulinzi bila ya kuchukuwa uhai wa mtu?
Hapana shaka yoyote kwamba kifo cha Daudi Mwangosi kimegubikwa na utata wa kutosha kuanzi mwazo hadi mwisho wa maisha yake, na hasa ukizingatia kwamba tukio hilo la mauaji limefanyika hadharani wakati  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Nd.Michael Kamuhanda alikuwa anatambua uwepo wa Daud Mwangosi  na pia umuhimu wa habari hizo kwa taifa, na kibaya zaidi ni pale kumuona Daud akiwa anafia kwenye mikono ya jeshi la polisi kulikoni?
Ikumbukwe kwamba siku zote hata katika vita waandishi wanafanya kazi bega kwa bega na askari ili kuwajuza wananchi nini kinachotokea na kinachoendelea kwenye uwanja wa mapambano.
Kutoka na kifo hicho ZPC inaomba hatua za kisheria zichukuliwe kwa wale wote waliohusika moja kwa moja na kifo cha mwandishi huyo.
Zanzibar Press Club kwa saa ingependa kuona utekelezaji mzuri wa kisheria kwa askari wote ambao walihusika kwenye kadhia hii.
Mbali na hayo, ZPC inawaomba waandishi wa habari wote wa Zanzibar wawe makini wakati wanapotekeleza majukumu yao, kwani kutokana na tukio hili limetufanya tuone kuwa Jeshi la Polisi ni Mdau anayetutia shaka katika utekelezaji wa majukumu yetu.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi Amini.
Abdalla Juma Pandu
Kaimu Mwenyekiti
Zanzibar Press Club

Wednesday, June 13, 2012

SMZ ipo pamoja na wananchi wake

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amesema viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katu hawatowasaliti wananchi wa Zanzibar katika kutoa maoni ya uundwaji wa katiba mpya ya Tanzania. 
Amesema viongozi wataheshimu na kutetea maoni ya wananchi wanatakayoyatoa kwenye Tume ya marekebisho ya katiba, na kutoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kutoa  maoni yao wakati utakapofika.
Maalim Seif ametoa kauli hiyo leo huko Eacrotanal Mjini Zanzibar alipokuwa akizindua kongamano linalohusu Muungano na Mchakato wa mabadiliko ya katiba ya Tanzania lililoandaliwa na kituo cha huduma za sheria Zanzibar.
Amesema kila mtanzania atakuwa huru kutoa maoni yake, na kwamba  ni fursa muhimu kwa Wazanzibari kueleza kero zinazowakabili ndani ya Muungano, badala ya kukaa kimya na kusubiri maamuzi yasiyokuwa na mustakbali mzuri na nchi yao.
Makamu wa Kwanza wa Rais amekiri kuwepo kwa kero nyingi za Muungano ambazo zinahitaji kutatuliwa kwa haraka ili kupunguza malalamiko ya wananchi wa pande mbili za Muungano.
Amefafanua kuwa kwa sasa yapo mawazo mengi kuhusu muundo wa Muungano, lakini amesema ni vyema kila nchi kati ya Tanganyika na Zanzibar ikawa na mamlaka yake kamili, kisha uanzishwe Muungano wa mkataba kwa mambo ambayo nchi mbili hizi zitakubaliana.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kituo cha huduma za sheria Zanzibar Profesa Chris Maina Peter amesema ni muhimu kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika kuunda katiba yao, ikizingatiwa kuwa katiba zilizopita hazikuwashirikisha wananchi moja kwa moja.
Nae Mwakilishi wa Shirika la Ford Foundation kanda ya Afrika Mashariki bwana Maurice Makoloo amesema shirika lake ambalo limekuwa likisaidia miradi mbali mbali ikiwemo kukuza demokrasia na kupunguza umaskini, litaendelea kushirikiana na Tanzania katika mchakato wake wa mabadiliko ya katiba ili kutimiza lengo lake la kukuza demokrasia katika nchi za Afrika Mashariki.
  Hassan Hamad (OMKR).

Tuesday, June 12, 2012

Tume ya taifa ya sayanzi yaombwa kuwahsjihisha wasomi

Uongozi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia Tanzania {costech} umeombwa kushajiisha Wasomi hasa Vijana wa Vyuo Vikuu Nchini kupenda kufanya tafiti mbali mbali zitakazojenga Mazingira ya kumuondoa  Mtanzania kwenye matatizo yanayomkabili.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ametoa ombi hilo katika Hafla fupi ya uzinduzi wa Ofisi ya Tume hiyo ilyofanyika hapo Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja.
Balozi Seif alisema Tafiti kama hizo ambazo zitakuwa na uhusiano wa moja kwa moja na Mwananchi  zinaweza kusaidia kupata Maendeleo kwa kasi zaidi katika Kipindi kifupi kijacho.
Alisisitiza kwamba Serikali kwa upande wake iko tayari kwa namna yoyote ile kutumia vyema matokeo ya Tafiti zinazofanywa na Wazomi wazalendo.
Hata hivyo Balozi Seif alieleza kuwa yapo baadhi ya matokeo ya Tafiti hubakia kuwa siri kwa Taifa lakini mengine yanastahiki kutolewa kwa Wananchi ili waelewe kinachoendelea kwenye maisha yao.
Balozi Seif alieleza kwamba wakati umefika kwa Makampuni pamoja na Viwanda vya hapa Nchini kujenga Utamaduni wa kutoa kazi zao za Utafiti kwa Tume hiyo ili ijipatie fedha za kuendesha shughuli zake za utafiti kama Nchi nyengine zilizoendelea.
Alieleza kwamba Tanzania imepania kuleta maendeleo kwa Wananchi wake kutokana na uamuzi wake wa kutenga Jumla ya shilingi za Kitanzania Bilioni Thalathini { 30,000,000,000/-} kwa ajili ya Utafiti na Maendeleo kwenye Bajeti yake ya Mwaka 2010/2012.
Balozi Seif alifahamisha kwamba Maendeleo bila ya Sayansi na Teknolojia  hayapatikani kwani masuala hayo mawili yanakaribiana katika utekelezaji wake.
Akizungumzia Tume ya Taifa ya nguvu za Atomu Balozi Seif  alielezea kufarajika kwake kutokana na mipango m,izuri ya Taasisi hiyo kuhudumia Zanzibar katika masuala ya usimamizi wa matumizi salama  ya Mionzi.
Balozi Seif alisema ushirikiano wa pamoja wa Taasisi hiyo,Wizara ya Afya Zanzibar na Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani katika kuanzisha  mradi wa Matibabu ya Saratani katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja unafaa kuungwa mkono.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameishukuru Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uamuzi wake wa  wa kusogeza karibu na Wananchi shughuli za  Ofisi ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia na Ofisi ya Tume ya Taifa ya  Nguvu za Atomu.
Katika Taarifa yake Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania Profesa Iddi Suleiman Nyangarika Mkilaha alisema Taasisi yake itaendelea kutoa Elimu sahihi ya matumizi ya Mionzi.
Profesa Nyangarika alisema Taaluma hizo kwa sasa itazingatia zaidi katika sekta ya Viwanda pamoja na Vituo vya Afya ambavyo vinatumia Vifaa vyenye mazingira ya Nguvu za Atomiki.
Mkurugenzi huyo wa Tume ya Nguvu za Atomiki alifahamisha kwamba katika kupanua zaidi huduma zake Taasisi hiyo itaendelea kupima Mionzi katika Mimea ili kujua kiwango sahihi cha kulinda Vyakula kwa ajili yamatumizi bora kwa Wanaadamu.
Mapema Waziri wa Mawasiliano,Sayansina Teknolojia wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Makame Mnyaa Mbarawa alisema Wizara hiyo itaendelea kushirikiana na Wataalamu wa ndani na nje ili kuona Tafiti zinazofanywa zinatmika kwa walengwa ambao ni Wananchi.
Alisema Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia na ile ya Nguvu za Atomiki zimeanzishwa zikiwa na wajibu wa kusimamia tafiti na nguvu za Atomiki Nchini kwa kushirikiana na Taasisi za Kanda na zile za Kimataifa.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Mkamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Friday, June 8, 2012

Msumbiji yakumbusha ufugaji wa samaki Zanzibar

Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa Msumbiji imekumbushwa tena kufikiria ombi la Zanzibar la kuipatiwa Wataalamu katika kuendeleza Sekta ya ufugaji wa Samaki wa Kamba.
Ombi hilo limetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wakati wa mazungumzo yake na Balozi wa Msumbiji Nchini Tanzania Bwana Zakaria Kupela yaliyofanyika hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alisema Msumbiji imekuwa na uzoefu wa muda mrefu katika shughuli za ufugaji wa kamba  na kujipatia umaarufu sehemu mbali mbali Duniani.
Alisema utaalamu na uzoefu ulioipata Nchi hiyo unaweza kuisadia Zanzibar katika moja ya harakati zake za kujenga mazingira ya ajira kwa Vijana wake.
“ Sio mbaya kukukumbusha tena lile wazo letu nililokuelezea  wakati ule tulipokutana kwa mara ya kwanza ingawa inaonekana kulikuwepo na tatizo la ufuatiliaji wa suala hilo”. Alisisitiza Balozi Seif.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alimpongeza Balozi Mdogo wa Msumbiji Bw. Zakaria Kupela kwa juhudi zake za kuendelea kuunganisha uhusiano uliopo kati ya Msumbiji na Tanzania na Zanzibar kwa Ujumla.
Balozi Seif alifahamisha kwamba uhusiano wa pande hizo mbili ni wa maumbile kutokana na maingiliano ya kidamu yaliyopo kati ya Wananchi wa Tanzania na Msumbiji.
Mapema wa Msumbiji aliyemaliza muda wake hapa Tanzania Bwana Zakaria Kupela alishauri rasilmali zilizopo kwa Mataifa yote mawili ni vyema zikawekewa mikataba kwa faida ya Vizazi vijavyo.
Balozi Kupela alisema Mataifa yote mawili yamebarikiwa kuwa na rasilmali nyingi mfano Maji,Madini, Gesi na Bahari ambazo kama hazikuwekewa utaratibu wa matumizi mazuri zinaweza kuchukuliwa na wajanja.
Alifahamisha kwamba Kizazi kijacho kinaweza kukumbwa  na ushawishi wa Baadhi ya Mataifa au mashirika ya Nje katika matumizi ya rasilmali hizo kinyume na  haki ya Mataifa husika.
Alisisitiza suala la kuendelezwa utaratibu wa kubadilishana Wanafunzi kati ya Tanzania na Msumbiji ambao utasaidia zaidi uhusiano wa pande hizo.
Balozi Kupela ameelezea faraja yake kuona nyanja hiyo imeshaleta matunda kwa vile tayari yapo mabadilishano ya wanafunzi 50 wa mwaka wa pili sasa kati ya Tanzania na Msumbiji.
Alisema mpango huo ukiandaliwa vyema unaweza pia kuratibu mafunzo yatakayowawezesha Vijana wa pande zote mbili hizo kuelewa vyema kizazi kilicholeta ukombozi kwa Mataifa hayo mawili.
Kuhusu suala la Amani Balozi Kupela aliwanasihi Wananchi wa Zanzibar kuendeleza amani waliyonayo ndani ya mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa  ambayo hivi sasa ni darasa kwa mataifa mengine Duniani.
Balozi Kupela alitahadharisha kwamba kitu chochote chenye cheche ya kutenganisha jamii ni hatari kwa faifa ya kizazi kijacho.
Balozi Kupela alifika Ofisini kwa Balozi Seif kuaga rasmi na kurejea Nyumbani Msumbiji baaada ya kumaliza muda wake wa Utumishi hapa Tanzania.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Wednesday, June 6, 2012

Mbaraka Juma Ali anatafutwa kwa kosa la wizi


   Mnamo tarehe 20 may 2012 siku ya jumapili ulifanyika wizi wa mali za ofisi ya zanzibar press club na mali za IS-HAKA OMAR RWEYEMAMU kwa mujibu wa polisi zinakadiliwa kuwa na thamani ya TSH.11,600,000 uliofanywa na kijana anayeitwa Mbaraka Juma Ali mkaazi wa zanzibar,wizi huo ulifanyika katika mtaa wa michenzani block no.7 ghorofa ya tatu mali zilizoibiwa ni pamoja na
                                   1.Radio aina ya panasonic
                                   2.kompyuta aina laptop
                                   3.sanduku   la nguo
                                   4.passport ya kusafiria
                                   5.dvd player.
                                   6.cheti cha kuzaliwa

Zanzibar yafundwa kuogelea

Mabingwa wa Kampuni inayojishughulisha na masuala ya Mafunzo ya upigaji mbizi na Uokozi ya Nchini Uingereza { In Deep Diver Training } na ile ya L&W inakusudia kuendeleza mafunzo ya uzamiaji kwa Vijana wa Taasisi tofauti hapa Zanzibar baadaye Mwezi wa Novemba mwaka huu wa 2012.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hizo Bwana Jim Kellett alieleza hayo wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo Nyumbani kwake Mazizini Nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Bwa Jim alisema mafunzo hayo yatawashirikisha Vijana 30 kutoka Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo KMKM, Shirika la Uvuvi wakiwemo pia wawakilishi wa Taasisi za Utalii.
Mkurugenzi huyo wa Kampuni ya Mafunzo na Huduma za upigaji mbizi alifahamisha kwamba Taasisi yake imeamua kuendesha Mafunzo kama hayo katika Nchi mbali mbali kwa lengo la kuwajengea uwezo Vijana wa kutumia Vipaji vyao katika Biashara ya upigaji mbizi.
Alisema mbali ya fani hiyo kutumiwa katika masuala ya uokozi lakini pia itasaidia kutoa ajira kwa Vijana waliomo ndani ya Sekta ya Utalii.
“ Sekta ya Utalii hivi sasa imechukuwa nafasi kubwa ya ya mapato na ajira Duniani. Sasa kuwapatia mafunzo ya upigaji mbizi vijana wanaojishughulisha na masuala ya Utalii ni kuwajengea uwezo mkubwa wa ajira ya kudumu kwao”. Alisisitiza Mkurugenzi huyo wa Kampuni ya L&W na ile ya In Deep Diver Taraining.
Bwana Jim ameelezea kufurahishwa kwake na mazingira mazuri aliyoyashuhudia hapa Zanzibar katika nyanja ya uzamiaji.
Aliishauri Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuzipitia Sheria na Kanuni za Uokozi kwa lengo la kuzifanyia marekebisho ili ziende na wakati wa sasa.
Naye Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliupongeza uongozi wa Kampuni zote mbili chini ya Mkurugenzi wao huyo kwa uamuzi wao wa kutoa Mafunzo ya Wiki mbili kwa Askari 30 wa Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo Zanzibar { KMKM }.
Balozi Seif alisema Mafunzo hayo Maalum ya uzamiaji yataweza kusaidia uokozi na hata Shughuli za Utalii hapa Nchini.
“ Uamuzi wenu wa kutoa Wataalamu wa kuendesha mafunzo hayo hasa kwa askari wetu wa KMKM unastahiki kupongezwa na Wananchi wote”. Alifafanua Balozi Seif Ali Iddi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliueleza uongozi wa Kampuni hizo kwamba Zanzibar inakusudia kufikia kuwa na Kiwango cha Kimataifa katika masuala ya Uzamiaji.
Alifahamisha kwamba Kiwango hicho kinakadiriwa kwenda sambamba na uanzishwaji wa Vituo visivyopunguwa sita vya huduma za Uokozi katika sehemu mbali mbali Unguja na Pemba.
Bwana Jim Kellett na Timu yake alikuwepo Zanzibar kuendesha mafunzo ya Wiki mbili kwa Askari 30 wa Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo Zanzibar {KMKM }.

Friday, March 23, 2012

Sheria ya Uvuvi Zanzibar

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inakusudia kuziangalia upya Sheria za Uvuvi zilizopo Nchini ili kuona uvuvi haramu ambao unaendelea kukithiri katika sehemu tofauti ndani ya Visiwa vya Zanzibar unaangamizwa kabisa.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alieleza hayo wakati akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Hifadhi ya Ghuba ya Menai katika Jengo la Ofisi hiyo liliopo Kizimkazi Wilaya ya Kusini.
Balozi Seif alisema katika kudhibiti wimbi hilo la Uvuvi haramu ameziagiza Kamati za Hifadhi ya mali asili za Baharini kuvichoma moto Vifaa vinavyokamatwa kutokana na Uvuvi huo maramu baada ya kuthibitishwa na Taasisi zinazohusika ya Masuala hayo.
Alisema hakuna mvuvi asiyeelewa nyavu haramu katika shughuli za Uvuvi lakini kinachojitokeza ni ile tamaa ya baadhi ya wavuvi hao ambayo ikiachiliwa inaweza kuvijengea mazingira ya hatari ya baadae vizazi vijavyo.
Balozi Seif alizipongeza Kamati za Hifadhi ya Mali asili ya Baharini hasa ile ya Ghuba ya Menai kwa juhudi zao za kulinda mazingira katika wakati mgumu.
Aliwataka kutovunjika moyo katika kujitolea huko na kuwaahidi kwamba Serikali itaendelea kushirikiana nao katika mapambano dhidi ya wavuvi haramu.
Mapema Katibu mtendaji wa Jumuiya ya Hifadhi ya Ghuba ya Menai Bwana Mohd Suleiman alisema wimbi la Uvuvi haramu hivi sasa linaonekana kuongezeka kwa kasi kwa kisingizio cha ukali wa Maisha.
Bwana Mohd ameiomba Serikali kuwa makini na watendaji wa Baadhi ya Taasisi za Serikali ambao hutumia mamlaka yao kuwapa nguvu Wavuvi haramu kuendelea kuchafua mazingira ya Bahari.
Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati hiyo Nd. Zahor Kamal Hassan alitanabaisha kwamba tabia ya baadhi ya wavuvi kuichezea bahari kwa kuendeleza tamaa ya haraka itapelekea kuiponza Jamii yote.
Mapema Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alitembelea Jumuiya ya Wafugaji nyuki iliyopo Muungoni { ZABA } ambapo Mtaalamu wa Nyuki Bwana Andrea Nolli alisema yapo mafanikio kiasi kutokana na mradi huo kuendeshwa kitaalamu.
Bw. Andrea alimueleza Balozi Seif kwamba juhudi za makusudi zinahitajika katika kulinda misitu kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa asali ambao unaonekana kupungua kutokana na ukatwaji ovyo wa Miti. Katika ziara hiyo ndani ya Wilaya ya Kusini Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alibahatika kuitembelea Redio ya Jamii iliyopo Mtegani Makunduchi 91.9 F.M na kuwataka Vijana hao wahakikishe kile wanachokitangaza kinapokelewa vyema na Wananchi.
Baadaye Balozi Seif aliangalia Skuli ya Migomba Kiongoni inayotowa mafunzo kwa wakulima wa Migomba pamoja na Shamba la Mihogo la Mkulima Salum Iddi ambapo alielezea kuridhika kwake na juhudi za wakulima hao katika kuimarisha sekta ya Kilimo kinachozingatia utaalamu wa kisasa.
Balozi Seif ambae pia Ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM aliweka jiwe la msingi la Mskani ya CCM ya Haturudi nyuma iliyopo Muyuni “C”.
Akiwapongeza Vijana hao kwa kuitikia wito wa CCM wa kujenga Ofisi za Matawi na Maskani zenye hadhi ya Chama Balozi Seif aliahidi kuchangia Mabati yote kwa ajili ya uwezekaji wa Maskani hiyo.
“Mkijenga Tawi au Maskani ya Chama cha Mapinduzi lazima ifanane na Chama Chenyewe” Alisisitiza Balozi Seif.
Balozi Seif alisema Chama cha Mapinduzi kinathamini kazi inayoendelea kufanywa na Wanachama wake ndani ya Mskani na Matawi Nchini kote.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

MESSAGE ON WORLD TUBERCULOSIS DAY 24 March 2012

For too long, tuberculosis has not received sufficient attention. The result of this neglect is needless suffering: in 2010 alone, nearly 9 million people fell ill with TB and 1.4 million died, with 95 per cent of these deaths occurring in developing countries. These numbers make tuberculosis the second top infectious killer of adults worldwide.
The impact reverberates far beyond the individuals directly affected. TB takes a heavy toll on families and communities. Millions of children have lost their parents. Children who are exposed to sick family members are at high risk of contracting the disease. Far too many go untreated, since TB is often difficult to diagnose and treat in children. That is why this year we should aim to expand awareness of how children are affected by the disease.
It is critical to support those who lack the means to respond with the care and treatment they need to enjoy healthy and productive lives.
With the right interventions, we can make a major difference. We know how to end all forms of TB, including multi-drug resistant TB – which has emerged in most countries – before it leads to severe manifestations that are costly to treat and cause additional suffering. Where we have taken strong and proven measures, the number of people falling ill with TB has declined markedly.
The World Health Organization reports that our concerted efforts have helped to cut death rates by 40 per cent since 1990. Forty-six million people have been cured and seven million lives have been saved since 1995 thanks to the efforts of the United Nations, governments, donors, civil society groups, private partners, public health experts, and tens of thousands of health workers and affected families and communities.
Now is the time to be even more ambitious and “Stop TB in our lifetime,” the theme of this year’s World TB Day.
I call for intensified global solidarity to ensure that all people are free from fear of tuberculosis and its devastating effects. Let us vow to end the neglect of TB and to end deaths from this disease in our lifetime.

ESSAGE ON THE INTERNATIONAL DAY FOR THE RIGHT TO THE TRUTH CONCERNING GROSS HUMAN RIGHTS VIOLATIONS AND FOR THE DIGNITY OF VICTIMS 24 March 2012

Today we pay tribute to the memory of Monsignor Oscar Arnulfo Romero, who was murdered in El Salvador on this day in 1980 for refusing to be silent in the face of violence, abuse and injustice.
The International Day for the Right to the Truth Concerning Gross Human Rights Violations and for the Dignity of Victims is also a time to laud the brave individuals across the world who have devoted their lives to the protection and realization of human rights despite the many grave risks that their work all too often entails.
The dramatic and transformational events of the past year, marked by widespread popular uprisings against long-entrenched dictators, showed yet again the acute need to preserve and reveal the truth about human rights violations committed during periods of repression and conflict. To deny victims this vital knowledge is to deny them justice, dignity and recognition of – as well as reparations for – their suffering and loss.
The implications reverberate well beyond individuals who have been directly affected by attempts to cover up human rights abuses. The rights to truth and justice are central to ending impunity for gross violations of human rights. In cases of enforced disappearance, families have the right to know the fate and whereabouts of their loved ones. In all instances, honouring this right puts others on notice that violations cannot stay hidden for long.
I am proud that the United Nations supports a range of truth-seeking mechanisms that can play a powerful role in documenting gross human rights violations, including truth and reconciliation commissions, international commissions of inquiry and fact-finding missions. These are central to our quest for justice and stability.
I also welcome the recent decision by the United Nations Human Rights Council to appoint a new Special Rapporteur on the promotion of truth, justice, reparation and guarantees of non-recurrence.On this International Day, let us work to help all victims realize their right to truth and to protect all those who fight to see the truth prevail.

Thursday, March 22, 2012

Balozi Seif atowa mkono wa pole kwa Ubalozi Mdogo wa Misri

Waumini wa Dini ya Kikristo wa Madhehebu wa Coptic Orthodox Church Nchini Misri wanaendelea na Maombolezo kufuatia kifo cha Kiongozi wao Pope Shenouda wa tatu.
Pope Shenouda amefariki Dunia usiku wa Jumamosi ya Tarehe 17 Mach mwaka huu Nchini Misri Taifa lenye Waumini wa Dhehebu hilo la Coptic wapatao Milioni nane.
Hapa Zanzibar Viongozi na makundi ya Waumini wa madhehebu tofauti wamekuwa wakiweka saini kitabu cha maombolezo kwenye Ofisi ya Ubalozi wa Misri uliopo Vuga Mjini Zanzibar kufuatia kifo hicho.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alikuwa miongozi mwa watu mbali mbali walioweka saini kitabu hicho cha Maombolezo ya Popa Shenouda 111 Nchini Misri.
Akitoa salamu zake ya rambi rambi kufuatia kifo hicho Balozi Seif alimuomba Balozi Mdogo wa Misri aliyepo Zanzibar Bw. Walid Ismail pamoja na Waumini wa Dini hiyo Nchini Misri kuwa na moyo wa subra kutoklana na msiba huo mzito.
Naye Balozi Mdogo wa Misri aliyepo hapa Zanzibar Bwana Walid Ismail alieleza faraja yake kutokana na Wananchi wa Zanzibar kuguswa kwao na msiba huo.
Pope Shenouda 111 amezaliwa tarehe 3 Agosti mwaka 1923 katika Mji wa Alexadria Nchini Misri na kupata elimu ya msingi, Sekondari hadi chuo Kikuu katika fani ya Historia.
Ametumikia wadhifa huo wa pope Wa Alexadria tokea Tarehe 14 Novemba mwaka 1971 hadi kufariki kwake akijihusisha pia katika masuala ya Uandishi, Ualimu pamoja na kuhamasisha suala la amani miongoni mwa waumini.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Wednesday, February 29, 2012

WATU WENYE KUISHI NA ULEMAVU

Na Is-haka Omar ZPC
Kwa miaka mingi sasa ,suala la ulemavu halikuwa na umuhimu wowote katika jamii kutokana na mitizamo na imani potofu ingawa ulemavu umekuwa ukiongezeka siku hadi siku kutokana na sababu za kiuchumi,kisiasa ma kijamii.
Suala hili limeanza kuzungumzwa baada ya mwaka wa kimataifa wa watu wenye ulemavu (1981)ambapo umoja wa mataifa na jumuiya za watu wenye ulemavu dumiani zilipoanza kutetea ulemavu kama suala la haki ya binadamu.
Katika takwimu za kimataifa zinabainisha kuwa zaidi ya watu bilioni 1.5 wanapata ulemavu kila mwaka kupitia vyanzo mbalimbali vya kimaisha, lakini idadi hiyo inashamiri zaidi katika nchi zenye migogoro ya kivita kwani nchi hizo zinakuwa na watu wengi wenye ulemavu.
Tunatakiwa kufahamu maana ya ulemavu pamoja na kutofautisha aina hizo na viwango vya ulemavu,na kuelewa sababu za mtu kupata ulemavu katika kuelimisha jamii jinsi ya kujikinga na ulemavu sambamba na kuelewa changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu kidunia.
Tukumbuke kuwa ulemavu ni athari ya muda mfupi au ya kudumu inayosababishwa na hitilafu za kiwiliwili au hisia mfano uoni,usikivu,akili,kusema na kumsababishia mtu kushindwa kufanya kazi kikawaida.
Katika uchambuzi wa makala hii umebainisha aina kuu za ulemavu kuwa ni pamona ulemavu wa viungo,ulemavu wa uoni,kiziwi na matatizo ya kusema,ulemavu wa akili,albino (ulemavu wa ngozi) mwingineo kama kifafa,kichwa kikubwa mpasuko wa mdomo pamoja na ulemavu mchanganyiko ambapo mtu anakuwa na ulemavu zaidi ya mmoja.
Pia ulemavu umegawanyika katika viwango tofauti kuna ulemavu mdogo huu mtu anakuwa hitilafu au kasoro ndogo katika mwili au hisia lakini anaweza kujihudumia na kufanya kazi zote,lakini upo ulemavu wa kiasi mtu anaweza kujihudumia na kufanya kazi endapo atatumia visaidizi na mazingira yanapoboreshwa katika kiwango cha ulemavu mkubwa mtu huitaji kusaidiwa katika maisha yake yote.
Zipo sababu nyingi mtu ambazo anaweza kupata ulemavu kama kurithi,vita,utumiaji ovyo wa dawa za kulevya,magonjwa kama shinikizo la damu,kisukari,homa kali,surua,ajali,kupigwa,huduma duni kwa mama wajawazito wakati wa kujifungua na kupata mimba kwenye umri wa chini ya miaka 18 au zaidi ya miaka 35.
Changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu hapa nchini ni pamoja na kubaguliwa kijamii,kisiasa na kiuchumi mambo ambayo yakuwa vikwazo juu ya maisha yao ya kila siku na kusababisha wao kujiona kama watu ambao hawana umuhimu au haki ya kuishi kama watu wengine.
Ukosefu wa haki za msingi kama elimu,ajira na tiba zinazohusiana na wao pia ni tatizo ambalo linakua kwa kasi kubwa katika jamii yetu, licha ya kutolewa kwa elimu tofauti juu ya haki na usawa kwa watu wenye ulemavu juhudi za serikali pamoja na asasi binafsi katika kuhamasisha jamii kuondokana na dhana mbaya juu ya watu hawa ambayo wengi wanaamini kuwa watu wenye ulemavu ni moja ya jamii ambayo inahitaji msaada wa kila mara jambo ambalo si sahihi bali wanahitaji kuandaliwa mazingira mazuri ya kuweza kujitegemea wenyewe au kupewa msaada wa kielimu kama ujasilia mali ili waweze kujikimu kimaisha bila ya kutegema msaada wa mtu au taasisi fulani.
Umbali wa huduma za msingi unachangia katika kukwamisha maendeleo ya watu wenye ulemavu kwani ushindwa kufikia huduma muhimu kwa kukosa usafiri unaoendana na mazingira halisi ya watu hao,hivyo kama ni wanafunzi ushindwa kufika katika skuli au vyuo kwa muda unaotakiwa hata sehemu zao za kutafuta riziki yaani kazi halali ambayo ni haki ya msingi kwa kila mtu ,kufikia sehemu hizo upata vikwazo katika usafiri ikiwa katika daladala na aina zingine za usafiri.
Katika suala zima la kiuchumi wengi wao hukosa vyazo vya kujiingizia kipato yaani fedha na kujikuta wanashindwa kupata huduma za msingi au kushindwa kufanya biashara kutokana na hitilafu za kimaumbile walizonazo,hivyo upelekea kutomudu gharama za kununulia visaidizi vya kuwasaidia katika maisha yao ya kila siku.
Mazingira yasiyofikika nayo ni kikwazo kikubwa kwa watu hawa kwani wanashindwa kufikia huduma muhimu za kibinadamu hususani sehemu za majengo ya kwenda juu yanayojengwa na serikali pamoja na taasisi binafsi kwa ajili ya kutoa huduma za kijamii lakini ujenzi huo ,unakuwa kinyume na matarajio kwa watu hawa pamoja na jamii inayotambua haki na usawa kwa binadamu wote,kwani ujenzi huo hauzingatii miundo mbinu au matakwa ya watu wenye ulemavu kutokana na hali waliyokuwanayo ya kimaumbile unakuwa usumbufu kufikia sehemu za juu ndani ya majengo hayo kwani hapana visaidizi vya kisasa vilivyowekwa kwa ajili ya watu hawa.
Unyanyasaji na ubakaji kwa watu hawa jamii inachukulia kama sehemu ya maisha ya watu wenye ulemavu jambo ambalo si busara katika maisha halisi ya wazanzibar nchi yenye sifa za kipekee katika uso wa kidunia kwa wema,heshima,busara ,imani na hekima kwa raia wa nchi hii iliyojaa nyingi amani imetawala kila sehemu ya nchi,lakini hili tujue kuwa ni jukumu la kila mtu kusimamia na kukemea vitendo hivyo viovu ambavyo vinafanyika ndani ya jamii yetu tusitafute nani mchawi juu ya suala hili bali kukae na kutafakali kwa kina jinsi gani kumaliza tatizo hili,vipo vitendo vinavyosikitisha mfano utakuta mtu mwenye ulemavu wa akili anapewa uja uzito na mtu asiyejulikana,kweli katiba ya nchi ambayo ni sheria mama ya nchi inafanya kazi ipasavyo kwa kuwawajibisha watu wanaofanya vitendo vya uzalilisha na ubakaji kwa watu wenye ulemavu kama sheria na kanuni za nchi hazitekelezwi sasa wakati umefika kwa kila mmoja wetu kubadilika kitabia katika kusimamia na kutekeleza mambo yote yanayowahusu watu watu hawa.
Sheria ya watu wenye ulemavu( haki na fursa) na.9 ya mwaka 2006 inasema `watu wenye ulemavu wanatakiwa kuwa na fursa iliyo sawa kwa manufaa ya taifa katika nyanja zote za kijamii na katika elimu,habari,mawasiliano na mazingira ya kimaumbile kama vile lugha ya alama,tafsiri kwa visiwi,kanda,maandishi ya nukta nundu,taarifa na vipindi vinavyotokana na kompyuta,tovuti na kuweka mpangilio wa mazingira halisi kama vile nyumba,majengo,usafiri na mitaa ili waweze kuifikia.
Pia baraza la taifa la zanzibar la watu wenye ulemavu lilianzishwa chini ya kifungucha 26 cha sheria hii kwa lengo la kusimamia haki na maslahi ya watu wenye ulemavu nchini.
Kwa mujibu wa sheria hii kila jamaa wa mtu mwenye ulemavu atakuwa na wajibu wa kutoa haki na fursa kwa mtu mwenye ulemavu atakayeshindwa kufuata masharti ya kifungu (1) cha kifungu hiki atakuwa ametenda kosa,pale itakapothibitika kwa jamaa ana jhatia ya kuacha kwa makusudi kutoa haki na fursa kwa mtu mwenye ulemavu,mahkama inaweza kwa maombi kutoka kwa mtu mwenye ulemavu au baraza kuamuru kwamba haki na fursa zitolewe kwa usawa.
Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu unatambua umuhimu wa misingi na miongozo ya sera iliyokuwemo ndani ya mpango wa vitendo wa dunia kuhusu watu wenye ulemavu na kanuni za kutoa fursa sawa katika ushawishi,uendelezaji,utengenezaji na kuthamini sera,mipango na hatua mbalimbali katika ngazi ya kimataifa,kikanda na kitaifa ili kutoa fursa sawa kwa watu wenye ulemavu.
Katika ibara ya 27 kwenye mkataba wa kimataifa unabainisha nchi zilizoridhia mkataba huo zinatambua haki ya watu wenye ulemavu kufanya kazi kwa misingi sawa na wengine hii inajumuisha haki ya kujipatia nafasi ya kumudu maisha kwa kufanya kazi walioichagua au kuibua katika soko la ajira na mazingira ya kazi yawe wazi,shirikishi na yanafikika na watu wenye ulemavu pamoja na kulinda na kukuza upatikanaji wa haki ya kufanya kazi,ikijumuisha wale waliopata ulemavu wakiwa kazini,kwa kuchukua hatua na sheria inayofaa.
Mwanaharakati wa masuala ya watu wenye ulemavu Zanzibar bw.Ali Saleh ameelezea hisia zake juu ya watu wenye ulemavu hapa nchini katika mafunzo ya siku tatu ya waandishi wa habari juu ya kutambua haki na usawa kwa watu hao amesema bado jamii inatakiwa kubadilika kitabia na kufuata kanuni na sheria za nchi ,pamoja na kutambua na kuheshimu haki za binadamu bila ya kuacha nyuma utamaduni halisi wa mzanzibar ,hayo ni mambo muhimu ya kuzingatia kwa kila mmoja wetu ili nchi yetu iwe miongoni mwa nchi zinazojali na kutambua haki na fursa kwa watu wenye ulemavu.
Bi, Zainabu Khamis Mohamed anaishi na ulemavu wa ngozi (albino) amesema suala la ulemavu ni kasoro ndogo za kibinadamu zinazoweza kutokea kwa binadamu yeyote,hivyo jamii iwashirikishe katika masuala mbalimbali nao wanaweza kushiriki katika ujenzi wa taifa kama watu wengine ni muhimu kuondokana na imani potofu kuwa watu hao hawawezi kufanya kazi au kupata elimu vitu ambavyo ni msingi wa maisha ya kila mtu.
Aidha ametoa wito kwa serikali pamoja na taasisi binafsi kushirikiana katika kuwawezesha kiuchumi ili waweze kujiajiri wenyewe kwani kufanya hivyo kutawasaidia katika masuala mbalimbali ya kujikwamu kimaisha na kuondokana na umasikini.
Kama Mwandishi wa makala hii nina machache kwa jamii kweli yapo matukio mengi ya kusikitisha na kutisha wanayofanyiwa watu wenye ulemavu,lakini mbaya zaidi vyombo vyenye dhamana ya sheria vipo kimya wakati sheria na mkataba wa kimataifa ipo lakini wahusika wanaofanya matukio hayo hawawajibishwi,je kama sheria hazitekelezwi jamii zilizochoka na unyanyasaji na uonevu zitakuwa na imani au uzalendo juu ya nchi yao, tubadilikeni kwani suala la ulemavu si la mtu au watu Fulani kila mtu ni mlemavu mtarajiwa kama si leo basi kesho yaweza ukawa mlemavu wahenga walinena “kama ujafa ujaumbika ”methali hii tuitafakali kisha turudi katika misingi ya dini zetu bila ya kuacha nyuma utamaduni na uhalisia wa maisha yetu ya kila siku.
Ushauri wangu kwa serikali sasa naweza kusema kwamba wakati umefika wa serikali kukunjua mbawa zake katika jamii na kusimamia ipasavyo haki ma fursa kwa watu wenye ulemavu ili nao,waweze kuondokana vilio vya muda juu ya ubaguzi,mateso,machungu yaliyopelekea kukata tamaa kwa walio wengi,ni muhimu kufikiria zaidi juu ya uwepo wa watu hawa wenye uwezo mkubwa wa kiutendaji wakiwezeshwa na kupewa mbinu za kujikwamua pia washirikishwe katika mambo mbalimbali ya kitaifa na kijamii.