Saturday, February 25, 2012

Msumbiji yaitaka Tanzania kufukiria njia ya kurudisha vikao vya pamoja

Na Is-haka Omar ZPC
Msumbiji imeiomba Tanzania kufikiria uwamuzi wa kurejeshwa tena utaratibu wa kuwa na vikao vya pamoja kati ya pande hizo mbili ambao ulilenga zaidi kuimarisha ujirani mwema.
Ombi hilo limetolewa na Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania Bw.Zakaria Kupella wakati alipofanya mazungumzo na makamu wa pili wa rais wa zanzibar balozi Seif Ali Iddi hapo ofisini kwake vuga mjini Zanzibar.
Amesema tanzania ilikuwa mstari wa mbele katika kusaidia ukombozi wa mataifa ya bara la afrika ikiwemo jirani yake Msumbiji hivyo ni vyema vikao vya ushirikiano vikafufuliwa kwa nia ya kulinda umoja na udugu wa sehemu hizi mbili.
Amesistiza kwamba yapo maeneo mengi ambayo wananchi wa pande hizo mbili wamekuwa wakishirikiana pamoja hasa ikizingatiwa kwamba nchi hizo zimepakana.
Balozi huyo amesema ni vyema ukaandaliwa utaratibu wa kuyaunganisha makundi ya vijana wa pande hizo mbili kujenga taifa katika mpango wa kujitolea.
Naye Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema uhusiano wa pande hizo mbili unafaa uelekezwe zaidi katika uchumi badala ya siasa ambapo ameiomba msumbiji kufikira wazo la kutoa wataalamu kuja zanzibar katika kutoa elimu katika sekta ya uvuvi wa kamba.
Balozi Seif amesema dunia imeshuhudia kiwango kikubwa cha bidhaa ya kamba inayozalishwa msumbiji na kusafirishwa nje ya nchi na kuipatia kipato kikubwa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment