Friday, February 24, 2012

Oman yasaidia Zanzibar kimatibabu

Na Is-haka Omar ZPC
Serikali ya Oman imekusudia kutoa msaada wa matibabu nje ya nchi kwa watoto kuanzia mwaka mmoja hadi miaka kumi na sita wanaosumbuliwa na ugonjwa wa moyo.
Waziri wa afya Mhe.Juma Duni amesema kuwa wagonjwa hao watapelekwa katika hospitali ya Narayana nchini india kuanzia mwazoni mwa mwezi ujao kwa gharama zitakazotolewa na serikali ya oman ambapo mgonjwa mmoja anakisiwa kugharimu kiasi ya dola elfu nne hadi tano.
Akizungumza na waandishi wa habari amesema hatua hiyo itakuwa ya kuendela ikiwa ni juhudi ya wizara hiyo katika kutafuta ufadhili wa matibau ya watoto ambapo katika hatua ya awali watoto kumi hadi ishirini watasafirishwa kwa ajili ya matibau zaidi.
Mhe Duni amefahamisha kuwa timu ya madaktari watatu kutoka hospitali ya Narayana wanaendelea na zoezi la kuchunguza watoto hao kisiwani pemba na kwa unguja watoto 73 wamegundulika kuhitaji matibabu zaidi.
Hivyo ameishukuru serikali ya oman kwa ufadhili huo baada ya kuelewa tatizo hilo ikiwa ni juhudi za kusadia kuimarisha ustawi wa afya za watoto nchini.

No comments:

Post a Comment