Saturday, February 25, 2012

Balozi Seif afanya mazungumzo na Balozi wa EU Tanzania

Na Is-haka Omar ZPC
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amefanya mazungumzo na Balozi wa Umoja wa Ulaya (E.U) nchini Tanzania Bw.Filiberto Ceriani.
Katika mazungumzo yao viongozi hao walielezea haja ya kuongeza ushirikiano kati ya pande hizo mbili na Bw.Filiberto amesema umoja wa ulaya umeandaa mpango wa kuzijengea uwezo jumuiya na taasisi za kiraia utakaogharimu karibu Euro milioni tatu.
Amesema mpango huo utaenda sambamba na utowaji wa mafunzo kwa watendaji wa sekta ya sheria ili kuwajengea mazingira bora ya uwajibikaji sekta hiyo.
Nae Balozi Seif amesema Zanzibar inaendelea kupiga hatua za maendeleo kufuatia uendeshaji wa mfumo wa serikali ya umoja wa kitaifa.
Hata hivyo Balozi Seif amesema bado yapo maeneo muhimu ya huduma za kijamii kama maji, elimu na afya hayajafikia kiwango kilicholengwa.
Hivyo amesema msaada zaidi unahitajika kutoka kwa taasisi na washirika wa maendeleo juhudi hizo za serikali za kuwaletea maendeleo wananchi.

No comments:

Post a Comment