Friday, February 24, 2012

Kiongoni watakiwa kuinua sanaa

Na Is-haka Omar ZPC
Katibu Mkuu Wizara ya Kazi,Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika Bi.Asha Ali Abdallah amekitaka kikundi cha sanaa cha skuli ya Kiongoni kuendeleza sanaa ya ngoma kwani vipaji vikiendelezwa hupelekea kuwa sehemu ya kujifunza na kupata ajira.
Hayo ameyaeleza wakati wa kukabidhi fedha taslimu sh.laki tano kwa kiongozi wa kikundi hicho cha sanaa huko ofisini kwake Mwanakwerekwe.
Amesema lengo la kutolewa kuwa fedha hizo ni kuendeleza kikundi hicho kiweze kukua kisanaa na kuinua vipaji vya wasanii.
Bi.Asha amefahamisha kuwa msaada huo umetolewa kufuatia ahadi alizotoa makamo wa pili wa rais Mhe.Balozi Seif Ali Idd katika uzinduzi wa soko la jumapili (sunday market) huko michenzani.
Nae mwalimu wa kikundi hicho Bw.Shaabani Naim Suleiman ametoa shukrani zake kwa makamo wa pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi kwa kutimiza ahadi yake pamoja na kuahaidi kuwaendeleza wasanii.
Kikundi hicho kima wanafunzi 15 na viongozi 3 na wanajishughulisha na ngoa za msewe,chaso na kurungu.
Pamoja na hayo kazi kubwa ya kikundi hicho ni kutoa elimu kwa jamii juu ya mambo mbalimbali kupitia sanaa ya ngoma ikiwemo utunzaji wa mazingira ,dawa za kulevya na ukimwi.

No comments:

Post a Comment