Friday, February 24, 2012

Skuli ya Kisiwandui kufaidika na mtandao wa teknolojia

Na Is-haka Omar ZPC
Mbunge wa jimbo la kikwajuni Mh.Hamad Yussuf Masauni amekabidhi hundi ya shilingi milioni mbili kwa kampuni ya milenium enginearing ya Dar-es-salaam kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha teknohama ndani ya jimbo hilo.
Akikabidhi hundi hiyo amesema ujenzi huo utajengwa kwa awamu ambapo awamu ya kwanza itagharimu shilingi milioni tano ambacho kitawasaidia wananchi kitajengwa ndani ya eneo la skuli ya Kisiwandui kitawawezesha vijana kujiingiza katika mtandao wa sayansi na teknologia.
Akizungumzia suala la uimarishaji wa barabara za ndani ya jimbo hilo mh masauni amesema wamo mbioni kuzifanyia matengenezo ili kuziweka katika hali ya kuridhisha.
Nae mhandisi kutoka kampuni hiyo Bw Ali Bakari Ali amesema kampuni hiyo inashughulikia miradi mbali mbali ya maendeleo ya wananchi ambapo kwa hapa watajenga kituo hicho cha teknohama ili kuendeleza elimu nchini.
Aidha amewataka wananchi kufuata taratibu za kisheria wakati wanapotaka kujenga pamoja na kupata ushauri wa kitaalamu ili kuepusha usumbufu unaoweza kujitokeza .

No comments:

Post a Comment