Wednesday, February 22, 2012

JUMMAZA yakusudia kuziweka nyumba za maendeleo Kilimani kuwa safi

Na Is-haka Omar ZPC Zanzibar
Katibu wa jumuiya ya uhifadhi wa mazingira na maendeleo Zanzibar JUMMAZA Bw Ramadhan Fadhil amesema jumuiya hiyo imedhamiria kulifanya eneo la nyumba za maendeleo kilimani kuwa katika hali ya usafi na salama .
Akizungumza na waandishi wa wahabari wa vyombo mbalimbali huko kilimani amesema hatua hiyo imekuja kufuatia eneo hilo kuwa katika hali isiyoridhisha na kuhatarisha maisha ya wakaazi wa eneo hilo .
Bw Ramadhan amesema tayari jumuiya yake imeshaanza kazi ya kuondoa taka zilizomo pembezoni mwa nyumba hizo na kusafisha majani yaliyopo kweye eneo hilo .
Amesema baada ya hatua hiyo wanatarajia kusafisha mitaro na kuchukua taka nyumba hadi nyumba zoezi ambalo linatarajiwa kuwa la kudumu
Aidha ameiomba serikali na taasisi binafsi kuunga mkono jitihada za jumuiya hiyo iweze kufanikisha kazi ya kuweka mazingira safi na salama

No comments:

Post a Comment