Na Is-haka Omar ZPC Zanzibar
Tume ya taifa ya uchaguzi NEC imesema maandalizi ya uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Arumeru mashariki pamoja na ule wa madiwani katika kata nane mbalimbali hapa nchini yamekamilika.
Mwenyekiti huyo wa tume hiyo Jaji Mstaafu Damian Lubuva akizungumza jijini DSM amesema hatua mbalimbali za maandalizi zimeshakamilika, ikiwemo kuanza kusafirishwa kwa baadhi ya vifaa ambavyo vitatumika katika uchaguzi huo.
Amesema pamoja na hatua hiyo chama ambacho hakijasaini sheria ya maadili ya uchaguzi, hakitoruhusiwa kushiriki katika kampeni za uchaguzi huo mdogo ambao unatarajiwa kufanyika aprili mosi mwaka huu.
Nae Mkurugenzi wa uchaguzi wa tume hiyo Bw.Julius Mlaba amesema kampeni za uchaguzi kwa upande wa ubunge katika jimbo la arumeru mashariki zimepangwa kuanza march 9, wakati zile za udiwani katika kata nane zitaanza march 6.
Aidha amesema katika uchaguzi huo NEC itahakikisha kwamba uchaguzi huo unasimamiwa na kufanyika kwa misingi ya uhuru na haki ili kuondoa hali ya manung’uniko miongoni mwa wapiga kura kutoka vyama vya siasa .
Tume ya taifa ya uchaguzi NEC imesema maandalizi ya uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Arumeru mashariki pamoja na ule wa madiwani katika kata nane mbalimbali hapa nchini yamekamilika.
Mwenyekiti huyo wa tume hiyo Jaji Mstaafu Damian Lubuva akizungumza jijini DSM amesema hatua mbalimbali za maandalizi zimeshakamilika, ikiwemo kuanza kusafirishwa kwa baadhi ya vifaa ambavyo vitatumika katika uchaguzi huo.
Amesema pamoja na hatua hiyo chama ambacho hakijasaini sheria ya maadili ya uchaguzi, hakitoruhusiwa kushiriki katika kampeni za uchaguzi huo mdogo ambao unatarajiwa kufanyika aprili mosi mwaka huu.
Nae Mkurugenzi wa uchaguzi wa tume hiyo Bw.Julius Mlaba amesema kampeni za uchaguzi kwa upande wa ubunge katika jimbo la arumeru mashariki zimepangwa kuanza march 9, wakati zile za udiwani katika kata nane zitaanza march 6.
Aidha amesema katika uchaguzi huo NEC itahakikisha kwamba uchaguzi huo unasimamiwa na kufanyika kwa misingi ya uhuru na haki ili kuondoa hali ya manung’uniko miongoni mwa wapiga kura kutoka vyama vya siasa .
No comments:
Post a Comment