Monday, November 28, 2011

Kombe la Mapinduzi Zanzibar

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema Mpango wa kuandaa Kombe la Mapinduzi Cup umelenga kukuza Michezo pamoja na kuimarisha Ujirani mwema ndani ya Mipaka ya Afrika Mashariki.
Balozi Seif ametoa kauli hiyo wakati akizindua Kamati ya Mapinduzi Cup yenye wajumbe kumi ikiongozwa na mwenyekiti wake Mohd Raza Hassan katika Ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Mjini Zanzibar.
Alisema mpango huu unaweza kuongeza kiwango cha Michezo ndani ya kanda hii endapo Wapenda michezo na wadau wote wataonyesha ushirikiano wao kwa kamati hii.
Balozi Seif alisisitiza kwamba Serikali haina budi kuiunga mkono Kamati hii ili kuona inafanikisha malengo iliyopangiwa.
“ Na hili nitahakikisha litatekelezwa kwa upande wa Serikali Mimi mwenyewe nitalisimamia kwa vile ndie Mtendaji Mkuu wa Serikali ”.
Alisisitiza Balozi Seif.
Aliipongeza Kamati hii kwa kuwa na wajumbe mahiri na ana matumaini ya kufanikiwa na Kamati hiyo na kuvuka kiwango cha ufanisi cha mwaka uliopita.
Akimkaribisha Balozi Seif Waziri wa Hahabi ,utamaduni, Utalii na Michezo Abdillahi Jihadi Hassan amesema Wizara ina matuimaini makubwa na Kamati hiyo kwa vile imeundwa kwa kuzingatia uwezo na uzoefu walionao.
Mapema Mwenyekiti wa Kamati ya Mapinduzi Cup Mohd Raza ameahidi kwamba Kamati yake itahakikisha inatekeleza vyema majukumu yake kwa mujibu wa matakwa ya wadau wa Michezo.
Raza alisema Kamati yao itaendelea kuzingatia zaidi huduma na burdani kwa wananchi katika mashindano ya michezo ya Mapinduzi Cup yatakayojumisha Pia Mpira wa Wavu { Netball } kwa kuzhishirikisha baadhi ya Timu za Tanzania na timu alikwa kutoka nje ya Afrika Mashariki.
Kamati hiyo iliyoundwa chini ya uwenyekiti wa Mohd Raza ina wajumbe kumi ambao ni Sherry Khamis, Ibrahim Makungu, Mwakilishi wa Jimbo la Rahaleo Nassor Jazira, Katibu Mkuu Wizara ya Habari utamaduni na Mchezo Ali Mwinyikai na Naibu wake Issa Mlingoti.
Wengine ni Ali Khalil Mirza, Taufiq Turky, Aboubakar Bagharesa pamoja na Farouk Karim ambaye ndie Mratibu wa Kamati hiyo.
Othman Khmis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Elimu ya juu Zanzibar

Taasisi za Elimu ya Juu Nchini zina wajibu wa kuhakikisha idadi ya wanafunzi wa Kike kuingia Vyuo Vikuu inaongezeka ili kukidhi mahitaji ya Jamii.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameeleza hayo kwenye mahafali ya tano ya Chuo Kikuu cha Arusha ambapo jumla ya wahitimu 600 wamemaliza masomo yao ya shahada ya kwanza na Diploma katika Fani za Biashara, elimu na Ustawi wa Jamii.
Balozi Seif alisema ongezeko hilo litaondosha kabisa pengo kubwa liliopo kati ya Wanafunzi wa Kike na Kiume katika Elimu ya Vyuo Vikuu hapa Nchini.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliuagiza Uongozi wa Chuo Kikuu cha Arusha kuongeza Mikakati madhubuti ili kuleta uwiano wa Wananfunzi wa Jinsia zote.
“ Tafiti zinaonyesha kwamba kumuelimisha Mwanamke sawa na kuwaelimisha watu kumi. Hii inamana kwamba familia itaelimika haraka iwapo kutakuwa na mmoja wa Mwanamke aliyepata elimu” Alisisitiza Balozi Seif Ali Iddi.
Alifahamisha kwamba vyuo Vikuu Vikuu lazima vishirikiane na Serikali katika kuona Dira ya Taifa ya Maendeleo ishirini ishiri
{ Vission 2020 } inafikia malengo yake.
Balozi Seif aliitaja changamoto inayowakabili wana vyuo Vikuu ni namna gain wanaweza kutumia Taaluma yao kushajiisha Sekta Binafsi katika kuibua ajira ndani ya Jamii.
Alisema hatua hiyo itakwenda sambamba na mipango ya Serikali zote mbili za kuandaa mazingira bora ya kuongeza fursa katika soko la ajira hasa kwa kundi kubwa la Vijana.
Katika risala yao iliyotolewa na Rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuoni hapo Nd. Joshua Onyango wameiomba Serikali kuwapunguzia matatizo yanayowakabili ya Ubovu wa Bara bara, Huduma za Maji safi pamoja na Huduma za Umeme.
Wamesema matatizo hayo kwa kiasi kikubwa yanachangia kupunguza ari yao ya kujipatia Taaluma kwa utulivu ambayo ndio lengo la kuwepo kwao Chuoni hapo.
Naye Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Arusha Dr. Laban Mgedi alisema lengo la chuo hicho ni kuongeza asilimia 32% ya wanafunzi wa kike Chuoni hapo.
Dr. Laban amefahamisha kwamba Afrika inahitaji wasomo wa fani tofauti wakiwemo wanawake ili kuleta Mapinduzi ya haraka ya Elimu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi katika Mahfali hayo pia aliweka jiwe la Msingi la Jengo la Michezo la Chuo hicho.
Jengo hilo linalotarajiwa kukamilika ujenzi wake mwezi Febuari mwakani linatarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi za Kitanzania Milioni mia mbili.
Kukamilika kwa jengo hilo kutatoa afuaeni kwa wanafunzi kuwa na darasa la uhakika la masuala ya Sanaa na Utamaduni chuoni hapo.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Saturday, November 26, 2011

Tubadilike kokomesha ajira za watoto

Inaonekana bado jamii haijataka kubadili tabia ya kukomesha ajira mbaya kwa watoto kama ambvyo mtoto alivyokutwa akifanya biashara za kitalii pembezoni mwa fukwe za bahari ya Bagamoyo, hii ni ajira mbaya zaidi kwani kwa asilimia mia moja mtoto huingia kwenye matatizo ya unyanyasaji wakijinsia n.k

Thursday, November 24, 2011

Bara la Afrika limefanikiwa katika kupunguza migogoro kwa kutumia mbunu mwafaka

Changamoto kubwa inayolikabili Bara la Afrika Hivi sasa katika kuelekea kwenye Maendeleo zaidi ni kutumia mbinu na Marifa yaliyopelekea kupunguza migogoro ya Kijamii katika baadhi ya Mataifa ndani ya Bara hili.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ametoa kauli hiyo wakati akifungua Mkutano wa Tatu wa Viongozi na Wataalamu wanaoshughulikia Kuondosha migogoro Barani Afrika unaofanyika huko katika Hoteli ya Melia iliyopo Pwani Mchangani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Balozi Seif alisema Jamii ya Kimataifa imeshuhudia utatuzi wa Migogoro kadhaa Barani Afrika hali ambayo kwa kiasi kikubwa imepunguza Migogoro na hata Mauaji ya Raia wasio na hatia. Aliwataka Viongozi na Wataalamu hao kutumia fursa nzuri iliyopo ya Amani iliyorejea Barani humu kwa kuweka Mipango bora itakayoleta faraja zaidi ya ustawi wa Jamii katika miaka ijayo.
“ Tumeshuhudia utulivu wa Kisiasa ilivyorejea ndani ya Bara hili hasa katika Ukanda wa Maziwa Makuu eneo ambalo Sudan na Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo { DRC } zilikuwa katika migogoro mikubwa ya Kisiasa ”. Alikumbusha Balozi Seif.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alielezea matumaini yake kwamba Ripoti itakayotolewa na Viongozi hao baada ya kumalizika Mkutano wao itawezesha kujenga mazingira bora ya kudumisha Amani Barani Afrika.
Balozi Seif amezipongeza Taasisi zilizoandaa Mkutano huo ile ya Mwalimu Nyerere, Kituo cha Hali za Binaadamu cha Kimataifa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Norway kwa uamuzi wao wa kufanya Mkutano huo Hapa Zanzibar na hasa ndani ya Jimbo lake ya Kitope.
Alisema uwamuzi wao huo haukuwa wa kubahatisha bali imekuja kwa kuzingatia sifa ya Zanzibar ya amani iliyopelekea kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa { GNU } kufuatia Mgogoro wa muda mrefu uliovihusisha Vyama vya CCM na CUF.
Balozi Seif aliwaeleza Washiriki wa Mkutano huo kwamba Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar inafanya kazi zake vyema huku ikikabiliwa na changa moto kubwa ya kutekeleza matarajio ya Wananchi wote wa Zanzibar.
Akimkaribisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Dr. Salim Ahmed Salim alisema yapo Maendeleo makubwa ya kupunguka kwa Migogoro Barani Afrika jambo ambalo limeleta faraja kwao akiitolea mfano nchi ya Sudan.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Kimataifa cha Haki za Binaadamu bwana David Harland ameipongeza Zanzibar kwa ukarimu wake unaopelekea kupokea Vikao na Mikutano Mzizito ya Kimataifa ndani na nje ya Bara la Afrika.
Wakati wa Mchana akiwa Mkoani Dodoma Makamu wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alikutana wa Uongozi wa Kampuni ya uwekezaji vitega uchumi inayojishughulisha na Mradi wa umeme unaotumia upepo na jua kutoka Nchini India.
Mkurugenzi mkuu wa Kampuni hiyo ya Indomount bwana sudhakar amesema Taasisi yake imepanga kutumia Jumla ya Dola za Kimarekani Bilioni Moja kati ya Bilioni saba zilizotengwa na waziri mkuu wa Nchi hiyo kusaidia Serikali na Taasisi Binafsi Barani Afrika.
Naye Balozi Seif ameuomba Uongozi wa Kampuni hiyo kuangali Meneo ambalo wanaweza kusaidia kati ya yale yaliyoainishwa na kupendekezwa na Zanzibar katika mipango yake ya Maendeleo.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Tuesday, November 22, 2011

Uongozi mpya wa Singida Press Club

Safu ya waliosimama nyuma ni Emmanuel Michael (Katibu Msaidizi), Abby Nkungu (Katibu Mtendaji), Seif Takaza (Mwenyekiti) na Rev Immanuel Barnaba (Mjumbe).
Walio simama safu ya mbele ni Nathaniel Limu (Mweka hazina Msaidizi), Joseph Lujuo (Mjumbe), Awilla Silla (Mweka Hazina)na Elisante John (Mjumbe).

Sunday, November 20, 2011

New leaders of Singida Press Club

THE Annual General Meeting of the Singida Press Club (SINGPRESS), has elected Seif Takaza, as a new Chairman for three years term with effect from November 18, this year.
Takaza has taken over from Rev Immanuel Barnaba who did not defend his title but opted for another post. Prior to the elections, Takaza was the Assistant Executive Secretary.
It was not an easy task for Takaza to acquire the prestigious post. A re-run voting had to be conducted after another candidate who was eyeing the same post, Damiano Mkumbo, tied points with him.
Abby Nkungu bounced back to leadership in style after staying on the sidelines watching for three years following his resignation in 2008. He was elected the Club’s Executive Secretary pushing aside miserably the incumbent Doris Meghji.
Awila Silla, the only lady in the SINGPRESS new lineup, was elected treasurer. Jumbe Ismael was elected Vice Chairman, Emmanuel Michael picked the Assistant Secretary and Nathaniel Limu , the clubs assistant treasurer.
Rev Immanuel Barnaba, Elisante John and Joseph Lujuo were elected members of the executive committee.
The AGM also fired from being SINGPRESS member, Hillary Shoo, after he was found guilty of gross misconduct and behaving contrary to journalistic code of ethics.
Opening the meeting, Singida Regional Commissioner Dr Parseko Kone called on all scribes in the region to uphold their professional ethics saying that would enable the community surrounding them hold the profession in high esteem.
He further asked the journals to be impartial and stick to professionalism by giving fair coverage to all and sundry without fear or favor.
The elections were presided over by the Singida Regional Social Welfare Officer, Zuhura Karya and witnessed by Assistant Programme Officer from Union of Tanzania Press Clubs (UTPC, Victor Maleko

New leaders of Singida Press Club

THE Annual General Meeting of the Singida Press Club (SINGPRESS), has elected Seif Takaza, as a new Chairman for three years term with effect from November 18, this year.
Takaza has taken over from Rev Immanuel Barnaba who did not defend his title but opted for another post. Prior to the elections, Takaza was the Assistant Executive Secretary.
It was not an easy task for Takaza to acquire the prestigious post. A re-run voting had to be conducted after another candidate who was eyeing the same post, Damiano Mkumbo, tied points with him.
Abby Nkungu bounced back to leadership in style after staying on the sidelines watching for three years following his resignation in 2008. He was elected the Club’s Executive Secretary pushing aside miserably the incumbent Doris Meghji.
Awila Silla, the only lady in the SINGPRESS new lineup, was elected treasurer. Jumbe Ismael was elected Vice Chairman, Emmanuel Michael picked the Assistant Secretary and Nathaniel Limu , the clubs assistant treasurer.
Rev Immanuel Barnaba, Elisante John and Joseph Lujuo were elected members of the executive committee.
The AGM also fired from being SINGPRESS member, Hillary Shoo, after he was found guilty of gross misconduct and behaving contrary to journalistic code of ethics.
Opening the meeting, Singida Regional Commissioner Dr Parseko Kone called on all scribes in the region to uphold their professional ethics saying that would enable the community surrounding them hold the profession in high esteem.
He further asked the journals to be impartial and stick to professionalism by giving fair coverage to all and sundry without fear or favor.
The elections were presided over by the Singida Regional Social Welfare Officer, Zuhura Karya and witnessed by Assistant Programme Officer from Union of Tanzania Press Clubs (UTPC, Victor Maleko

Volunter wa UTPC

Mwandishi wa habari kutoka Ujerumani Jenis Westphal ambaye yupo kwenye afisi za UTPC akifanya kazi za kujitolea kama mwandishi wa habari na mpiga picha kwenye afisi za UTPC zilizopo jijini Mwanza
Jenis Westphal akiwa afisini za UTPC Mwanza

Saturday, November 19, 2011

Friday, November 18, 2011

Makamo wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Sauti za Busara

Sauti za Busara Zanzibar yahitaji wafadhali wengi zaidi ili kuhakisha kwamba tamasha hili linaweza kuendelea zaidi na hasa katika kuimarisha Utamaduni wa Zanzibar pamoja na kukusa soko la Utaii visiwani Zanzibar

Thursday, November 17, 2011

mkutano wa Waandishi na Wadau wa Habari uliofanyika tarehe 08.10.2011, katika ukumbi waEACROTANAL Zanzibar, Mkutano huo uliandali na ZPC na UTPC

Waandishi wakiwa katika mkutano wa pamoja na wadau wa habari, mkutano ambao ulifanyika kawenye ukukmbu wa Eacrotanal Zanzibar

Katibu Mtendaji na Naibu Katibu wa ZPC wakiwa kwenye Mkutano wa wadau na waandishi wa habari
Waandishi na wahariri wa habari kutoka kwenye vombo mabali mbali wakifuatilia kwa makini mada ya Utawala bora kwenye vyombo vya habari kwenye mkutano uliowakutanisha waandishi na wadawa wa habari nchini

Waandishi na Wadau wahabari wakiwa wamesima pamoja katika kuwaombea dua ndugu na jamaa waliofariki kwenye ajali ya meli ya Mv Spice Islanders hivi karibu visiwani Zanzibar



Mkurugenzi wa Shirika la Utaangazaji la Zanzibar mwenye kipaza sauti akijibu maswali yaliyoulizwa na washiriki katika mkutano kati ya waandishi na wadau wahabari

Mjumbe kutoka kwenye jumuiya ya Zanzibar Youth Forum akichangia mada

Mtangazaji kutoka Chuchu Fm akichangia mada

Mtangazaji kutoka Bomba Fm akichangi mada

Katibu Mkuu wa PPC akichangia mada kwenye Mkutano wa wadau na waandishi wa habari



Mjumbe kutoka AIDNET Zanzibar akichangia mada

Mwakilishi kutoka katika Idara ya Ustawi wa Jamii akichangia mada


Mjumbe kutoka chama cha AFP akichangia madaMwandishi wa The Gurdian akichangia mada


Mwasilishaji mada, ambaye pia ni mshauri katika masuala ya habari

Mwenyekiti wa ZPC akifungua mkutano wa Wadau na Waandishi wa Habari, mkutano ambao uliendesha na kusimamiwa na ZPC na UTPC.Picha zote ma Haroub Hussein Khamis wa Zanzibar Press Club

Monday, November 14, 2011

Balozi Seif akiwa na wageni waliomtembelea afisini kwake




MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDDI AKISALIMIANA NA MJUMBE WA KAMATI YA SIASA NA KAMATI KUU YA CHAMA CHA KIKOMINISTI CHA CHINA CCP BW, LIU YUNSHAN ANAEONGOZA UJUMBE WA WATU 21 WALIOFIKA OFISINI KWA BALOZI SEIF ILIOPO MTAA WA VUGA MJINI ZANZIBAR BW LIU YUNSHAN AKISISITIZA JAMBO WAKATI WA MKUTANO WAKE NA MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDDI KATIKA MKUTANO HUO BALOZI SEIF AMESEMA KUWA JAMHURI YA WATU WA CHINA ITAENDELEA KUWA KIUNGO MUHIMU KATIKA HARAKATI ZA KUSAIDIA UCHUMI NA MAENDELEO YA TANZANIA
MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDDI AKISALIMIANA NA KATIBU MKUU WA MIKUTANO YA KIMATAIFA YA UKANDA WA MAZIWA MAKUU BALOZI LIBERETE MULAMULA ALIYEIKA OFISINI KWAKE VUGA MJINI ZANZIBAR


Sunday, November 6, 2011

100% yafunika Nungwi

Sherehe za maridhiano na umoja wa kitaifa zilizoandaliwa na taasisi ya Swahili Center zinaendelea kwa kasi ambapo kwa Ijumaa iliyopita, vikundi vya Nyota ya Umoja (Maigizo,Nungwi) na Mkota Ngoma (Mkoani, Pemba) vilirindima katika kijiji cha Nungwi, Unguja.
Katika onesho hilo ambalo lilifanyika katika Uwanja wa Skuli ya Nungwi, Wilaya ya Kaskazini A, Mkoa wa Kaskazini Unguja, wapenzi wa fani za sanaa za maonesho kutoka sehemu mbali mabli waliliminika na kujimwaga katika burudani hizo zilizoanza saa 10 alasiri.
Kundi la Maigizo la Nyota ya Umoja, maarufu kwa michezo yao kama vile ‘Dhulma Kafara’ na ‘Masikini naye Mtu’, walitoa burudani safi kupitia mchezo wa ‘Mchelea Mwana Kulia’ uliobeba maudhui ya umuhimu wa ushirikiano wa kuyalinda maadili ya KiZanzibari ndani ya jamii.
Nalo kundi la Mkota Ngoma kutoka Mkoani, walikonga nyoyo za wapenzi wa Ngoma na asili kwa kupiga ngoma zao za Msembwe, Unjunguu na Kumbwaya. Wengi waliohudhiria shehere hizo walivutiwa sana na umahiri wa kundi hilo katika kuzicheza Ngoma hizo.
Katika kuutambulisha mradi huo kwa waliohudhuria onesho hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Swahili Center Bw. Kheri Abdalla Yussuf, aliwajulisha wapenzi hao wa sanaa za utamaduni kuwa dhamira ya mradi huo ni kuimarisha misingi ya umoja wa kitaifa nchini Zanzibar kupitia sanaa za utamaduni zenye burudani na mafunzo kwa jamii yote.
Wakati huo huo, aliyekuwa mgeni rasmi katika onesho hilo, Mhe. Bi Riziki Juma Simai (Mkuu wa Wilaya ya Kasakazi A) aliwataka wananchi wa Nungwi na wote waliohudhuria kuimarisha misingi ya umoja wa kitaifa kwa vitendo.
Mradi wa 100% Zanzibari (tafsiri; Mzanzibari asilimia mia moja) umekuwa ukifanya maonesho katika Mikoa ya Unguja na Pemba kufuatia kambi za kisanii zinazoshirikisha fani za Taarab, Ngoma za Utamaduni na michezo ya Kuigiza. Shangwe hizo zimekuwa zikifanyika kwa awamu katika sehemu mbali mbali ambapo kwa kipindi cha Nov 15-19 zitahamia katika Mkoa wa Mjini Maghribi.
Swahili Performing Arts Center (Kituo cha Sanaa za Maonesho cha Waswahili) ni taasisi ya iliyoanzishwa kwa dhamira ya kuchangia katika maendeleo ya sanaa za maonesho asilia za Zanzibar pamoja na zile za mwambao wa Waswahili kupitia uwezeshaji (wasanii), uzalishaji wa kazi za sanaa, maonesho na ushirikishaji jamii. Dira ya Swahili Center ni kuurejeshea hadhi utambulisho wa utamaduni wa Kiswahili.
Mradi wa 100% Zanzibari umedhaminiwa na Ubalozi wa Norway pamoja na kampuni ya mawasiliano ya Zantel.
Kheiri A.Y. Jumbe
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji

Robert Shumake akubali ombi la Balozi Seif Ali Iddi

Mamlaka ya Mitaji na Mendeleo ya Jamii ya wa Michigan Nchini Marekani imekubali kuisaidia Zanzibar katika masuala ya Elimu, Afya na Mazingira.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Bwana Robert Shumake ametoa kauli hiyo wakati wa mazungumao yake na makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi mwishoni mwa ziara yake Nchini Marekani.
Bw. Shumake ambaye tayari ameshakutana na Uongozi wa Benki ya Watu wa Zanzibar PBZ ambao umenambatana na Balozi Seif katika ziata hiyo mamlaka hiyo inajitayarisha kuongeza misaada yake kwa Tanzania ikiwemo Zanzibar.
“ Tumeshatoa misaada ya vifaa vya elimu kwa Nchi za Bara la Afrika ikiwemo Ethiopia na Tanzania katika skuli za Mkoa wa Kilimanjaro” Alisema Bwana Shumake.
Alisisitiza kuwa Mamlaka yake imekuwa ikitoa fursa za kudhamini masomo ya elimu ya juu kwa wanafunzi wa Afrika wenye mazingira magumu.
Bwana Shumake alisema utafiti uliofanywa na Mamlaka yake umegundua watoto wengi wa Bara la afrika wanashindwa kuendelea na Masomo ya juu kutokana na kukabilkiwa na umaskini uliokithiri.
Alimueleza Balozi Seif kwamba bado wanaangalia uwezekano wa kutoa huduma katika sekta za Kilimo ikilenga zaidi vijana ambao kundi kubwa linakosa ajira na kujikimu kimaisha.
Naye Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif ameipongeza Mamlaka hiyo kwa uwamuzi wake wa kusaidia huduma za kijamii.
Balozi Seif alisema Familia nyingi hasa za kiafrika zimekuwa zinakosa huduma za kijamii na kukumbwa na maradhi. Balozi Seif na Ujumbe wake unaondoka Marekani na unatarajiwa kuwasili nchini jioni ya Jumatatu ya tarehe 8/11/2011.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanziba

Zanzibar yashauriwa kuwatumia vyema waatalamu wake

Zanzibar imeshauriwa kuangalia njia za kuwatumia vyema Wataalamu Wazawa walioko nje ya Nchi ili kuharakisha kasi ya Maendeleo ya Jamii .
Ushauri huo umetolewa na Kiongozi wa Wazanzibari waliopo Nchini Marekani ambao wako katika hatua za mwisho kuandaa Jumuiya itakayoitwa Zanzibar Diascora Organization Dr. Omar Haji Ali wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozo Seif Ali Iddi kwenye Hoteli ya Crown Plaza Mjini Washington DC. Nchini marekani.
Dr. Omara alimueleza Balozi Seif kwamba lengo la Jumuiya hiyo ni kuunganisha nguvu kati yao na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kuona kwamba uwepo wao nje ya Zanzibar unaleta faida kwa Jamii yote. Alisema hivi sasa wanakamilisha taratibu za kuwaunganisha wenzao wa miji tofauti ili ifikapo Januari mwakani Jumuiya yao ianze kazi rasmi.
“ Tumefanya utafiti na kugundua Wapo Wazanzibari wengi wenye sifa na uwezo mkubwa kitaaluma ambao wanaweza kuitumia na kusaidia nyumbani ”. Alisema Dr. Omar.
Alisisitiza kwamba taratibu zinaandaliwa za akuwaunganisha Wazanzibari wengi walioko katika Jumuiya za Uingereza na Canada kwa ania ya kuwa na kiungo muhimu kati yao na Zanzibar hasa katika maeneo ya Uwekezaji na Uatafiti katika Sekta tafauti.
Alisema kuanzishwa kwa mawasiliano ya moja kwa moja yatatoa fursa kwa wenye nia ya kusaidia kupitia jumuiya hiyo. Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibarf Balozi Seif Ali Iddi ameipongeza azma yan Jumuiya hiyo ya Zanzibar Diascora Organization na kuahidi kuipa Baraka.
Balozi Seif alisema Serikali inaunga mkono vikundi vya Diascora na kuvitaka kuwa karibu na Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania.
“ Serikali ya SMZ tayari imeshaundan Idara inayosimamia Diascora kwa lengo la kuwaunganisha wazawa walioko nje ya Nchi. Hivyo tutahakikisha mnakuwa na mawasiliano ya karibu na Taasisi hii “ Alisema Balozi Seif Ali Iddi.
Othmana Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Friday, November 4, 2011

Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na Wanajumuiya ya Afrika ya Mashariki waishio Marekani

Wana Jumuiya ya Afrika Mashariki wanaoishi Florida Nchini Marekani wameombwa kuendelea kushirikiana pamoja kwa lengo la kutatua matatizo wakati yanapotokea na kuwazunguuka.
Ombi hilo limetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Mjini Tallahassee Jimbo la Florida Nchini Marekani baada ya kushiriki katika chakula cha pamoja na Wana Jumuiya hao.
Balozi Seif alisema matatizo mengi yanayowakabili wanaadamu yanashindwa kupatiwa ufumbuzi kutokana na kukosekana kwa ushirikiano wa pamoja.
“ Wana Jumuiya nyinyi ni vyema mkapendana na kushirikiana kwa vile mko mbali na familia zenu mnazozitegemea. ”. Alisema Balozi Seif Al Idi.
Amewataka kufuata Sheria na taratibu zilizowekwa Nchini humo ili kuepuka adhabu inayoweza kuwaletea balaa katika mfumo wa maisha yao ya kila siku.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif amewapongeza wana jumuiya hao wa Afrika Mashariki wanaoishi Florida Marekani kwa uwamuzi wao wa kuunda umoja wao unaosaidia kusukuma mbele maisha na Maendeleo yao.
Hata hivyo amewakumbusha hatma ya maisha yao ya baadaye ambayo inahitaji kufanyiwa maandalizi ya msingi.
Balozi Seif alisema haipendezi kuona mwana Jumuiya anafanya kazi ughaibuni lakini hatma ya maisha yake arudipo nyumbani inavunja moyo.
“ Inakua karaha unarudi ughaibuni na kutaka kuishi kwenye nyumba ya mjomba. Huko ni kujidhalilisha na kujimaliza kimaisha ”. Alitahadhaisha Balozi Seif Ali Iddi.
Umoja wa Wanajumiya ya Afrika Mashariki ulioanzishwa karibu miaka saba iliyopita Umejumuisha pia Wanachama kutoka Mataifa ya Carribean na Nigeria.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yassaini mkataba wa mashirikiano katia yake na chuo cha ufundi cha Florida

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetiliana Saini Mkataba wa Mashirikiana kati yake na Chuo Kikuu cha Kilimo na Ufundi cha Florida { FAMUJ } Nchini marekani.
Mkataba huo una lengo la kubadilishana uzoefu na Utaalamu kati ya chuo hicho na chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar { SUZAZ}.
Utiaji saini huo umefanyika katika Majengo ya Chuo hichocha Florida yaliyopo katika mji wa Tallahassee ambapo kwa upande wa Zanzibar umewakilishwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na ule wa Florida umewakilishwa na Rais wa Chuo hicho cha
{ FAMU } Dr. James ammons.
Akizungumza katika hafla hiyo iliyoshuhudiwa pia na wanafunzi wa fani fofauti chuoni hapo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameshauri taaluma inayotolewa na chuo kikuu cha Florida iingie katika nchi changa ili kuleta mabadiliko ya kilimo na ufundi.
Balozi Seif alisema Mataifa mengi yanayoendelea hasa yale ya Bara la Afrika bado yanashindwa kukabiliana na changamoto zinayoyabaliki licha ya kwamba Mataifa hayo yanategemea Kilimo kwa asilimia zaidi ya 70%.
“ Florida University iwe kiungo cha kuunganisha Taaluma katika vyuo vikuu vya nchi changa kikiwemo kile cha suza ”. Alisema Balozi Seif.
Mapema Rais wa Chuo Kikuu cha Kilimo na Ufundi cha Florida
{ famu } Dr.James Ammons alisema Chuo hicho kinalenga kujenga nguvu ya Taaluma katika kuona kizazi cha sasa kinapata Elimu inayokwenda sambamba na mabadiliko ya kasi ya Sayansi na Teknolojia Duniani.
Dr. ammons alisema Chuo hicho kilichoanzishwa miaka 125 iliyopita kimefungua masomo ya Taaluma ya Madawa na Sheria yakianguliwa nay ale ya Kilimo na Ufundi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alipata fursa ya kukitembelea kitengo cha Ufundi cha Chuo hicho cha Florida
{ FAMU -FSU }.
Mkuu wa Kitengom hicho cha ufundi Dr. Regional Perry alimueleza Balozi Seif na ujumbe wake hatua waliyofikia chuoni hapo ya kifanya utafiti katika masuala ya Madawa na Wanaadamu.
Dr. Perry alisema wataalamu wa chuo hicho tayari wamefikia hatua ya kutengeneza Injini za vyombo vya moto.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Balozi Amina Salum Ali akizungumza na Balozi Seif Ali Iddi

Mwakilishi wa Bara la Afrika katika Umoja wa Mataifa Balozi Amina Salim Ali amewataka Watanzania kulitumia vyema soko la Marekani katika kukuza uchumi wa Taifa.
Balozi Amina alitoa nasaha hizo wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na Ujumbe wake ulipomtembelea Ofisini kwake Mjini Washington DC Nchini Marekani.
Amesema Marekani kupitia mashirika na makampuni kadhaa ya Nchi hiyo hivi sasa yameelekeza nguvu katika kuwekeza Vitega Uchumi kwenye Mataifa kadhaa Ulimwenguni.
“ Hakikisheni Watanzania mnachangamkia vyema fursa hizo ambazo wenzetu wa Nigeria, Ethiopia na hata Majirani zetu wa Kenya wanazitumia ”.Alisema Balozi Seif.
Balozi Amina ameziasa taasisi zinazosimamia uwekezaji kuwa makini na wawekezaji wanaoonyesha hamu ya kutaka kuwekeza.
Amesema si vyema kwa wawekezaji hao kuhangaishwa wakati wanapotaka kuwekeza vitega uchumi vyao Nchini.
Balozi Amina ameupongeza Ujumbe huo wa Zanzibar unaofanya ziara Nchini Marekani kwa hatua yake ya kuitangaza Zanzibar kwa wawekezaji wa Marekani kufungua milango ya uwekezaji Zanzibar.
Naye Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar balozi Seif Ali Iddi alimshukuru Balozi Amina kwa kuwa kiungo muhimu cha mawasiliano kati ya Zanzibar na Wawekezaji wa Marekani.
Balozi Seif alisema Mwakilishi huyo wa Bara la Afrika katika Umoja wa Mataifa amechangia kuifanya ziara hiyo kuwa ya mafanikio kwa kiwango kikubwa.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Utafiti wa mradi wa samaki Zanzibar na Marekani

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Taasisi ya Ushirikano ya Jimbo la Houston,Texas Nchini Marekani zimefikia hatua ya kukubaliana kufanya utafiti wa pamoja utakaopelekea kuanzishwa kwa Mradi mkubwa wa Samaki Zanzibar.
Hatua hiyo ya makubaliano imekuja kufuatia Kikao cha pamoja kati ya Ujumbe wa Zanzibar ulioko Nchini Marekani Kujitanga kwa wawekezaji wa Nchi hiyo ukiongoza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na ule wa Taasisi inayoratibu Miradi mikubwa ya Samaki Nchini Marekani ya { GRI } ikiongozwa na Rais wa soko la Kimataifa la Taasisi hiyo Bwana Tomas Newland.
Mazungumzo hayo yamefanyika hapo katika Afisi za Taasisi hiyo kwenye Jimbo la Houston, Texas Nchini Marekani.
Bwana Tomas Newland aliueleza ujumbe huo wa Zanzibar kwamba mradi huo mkubwa una uwezo wa kutoa ajira kwa Wananchi zaidi ya thalathini elfu.
Alisema miradi kama hiyo ambayo tayari imeshaanzishwa katika baadhi ya Mtaifa ya Afrika,Asia, Marekani na Ulaya inazingatia zaidi uhifadhi wa Mazingira pamoja na utoaji wa mafunzo kwa Wavuvi na Wakulima wa maeneo ya Vijijini.
“ Miradi kama hii ambayo hufadhiliwa na Taasisi za Uwekezaji Vitega Uchumi za OPIC na IFC hugharimu zaidi ya Dola za Kimarekani Milioni 20,000,000.
Kwa upande wake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameshauri kuharakishwa kwa mawasiliano ya pamoja kati ya wataalamu wa pande hizo mbili ili kuona wazo hilo la muelekeo wa kuanzishwa kwa mradi mkubwa wa Samaki linafanikiwa.
Balozi Seif alisema kuanzishwa kwa mradi huo mbali ya kuleta uhusiano wa karibu kati ya Zanzibar na Marekani lakini pia utaleta faraja kwa Wananchi walio wengi kujipatia ajira ya uhakika.
Mapema asubuhi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alikuwa na mazungumzo na Seneta wa Jimbo la Houston,Texas Bwana Rodey Ellis.
Katika mazungumzo yao Senata Rodney aliiponhgeza Zanzibar kwa juhudi zake za kharaisha Maendeleo ya Kiuchumi.
Seneta Rodney Ellis amemkabidhi Balozi Seif Ali Iddi na Ujumbe wake hati Maalum inayompa heshima ya kuwa mkaazi wa Jimbo la Houston, Texas.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Zanzibar yashuriwa kulitumia vizuri soka la Afrika ya Mashariki

Zanzibar imeshauriwa kulitumia vyema soko la Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika Mashariki kwa lengo la kukuza uchumi wake na kuondokana na kutegemea zao moja la karafuu kama mhimili wa Taifa.
Ushauri huo umetolewa na Mkamu wa Rais wa Shirika la uwekezaji Vitega Uchumi la Kimataifa Nchini Marekani { OPIC } Bibi Mimi Alemahou wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo Makao Makuu ya Shirika hilo Mjini Washington DC Nchini Marekani.
Bibi Mimi alimueleza Balozi Seif na ujumbe wake ulioko nchini Marekani kwa ziara ya Kikazi ya
kuitangaza Zanzibar kwa wekezaji kuwekeza Zanzibar kwamba Shirika hilo tayari limeshaandaa mpango wa kuwekeza ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki likilenga kusaidia eneo hilo Kiuchumi.
Alisema mpango huo una nia pia ya kuijumuisha Sudan ambayo imekuwa ikikabiliwa na ukame wa mara kwa mara licha ya kwamba haimo ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki { EAC }.
“ Tumelenga zaidi kuisaidia Sekta Binafsi kwa vile jamii kubwa hasa ndani ya Bara la Afrika imekuwa ikikabiliwa na Uchumi duni ”. Alisema Bibi Mimi Alemayehou.
Bibi Mimi alifahamisha kwamba huduma za Shirika hilo la OPIC mara kahaa huelekezwa katika kutoa huduma za Kijamii kwenye sekta Binafsi kupitia Makampuni ya Kimarekani Chini ya Shirika la Misaada la Marekani US aid.
Naye Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar balozi Seif Ali Iddi ameuambia Uongozi wa Shirika hilo la Uwekezaji Vitega Uchumi la OPIC kwamba Zanzibar bado inaendelea kutegemea zao moja tu la Uchumi la akARAFUU.
Balozi Seif alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iko katika harakati za kuimarisha miundombinu ili kuyawezesha Makampuni ya Kigeni kupata fursa ya kuwekeza Zanzibar.
Alisema wawekezaji katika Sekta ya Utalii wana nafasi nzuri ya uwekezaji kwa vile miundo mbinu ya bara bara, maji na umeme iko katika hatua nzuri.
Hata hivyo Balozi Seif ameuomba Uongozi wa OPIC kuangalia uwezekano wa kuanzisha mradi wa pamoja wa umeme kwa kutumia Nishati ya jua au Bahari ili Zanzibar iwe tayari kukabiliana na upungufu wa huduma ya umeme hasa wakati kinapopungua kina cha maji huko Tanzania Bara.
“ Tumekuwa tukipokea huduma ya umeme kupitia Gridi ya Taifa huko Tanzania Bara, lakini wakati mwengine tunalazimika kupata umeme wa mgao kutokana na kupungua kwa kina cha maji. Hali hii huathiri utendaji kazi na kupunguza kasi ya Maendeleo ya Kiuchumi ”. Alisema Mkamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar. Balozi Seif.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Mkamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Thursday, November 3, 2011

Sanaa na wasanii

Mwambiji Amina wa Kikundi cha taarabu cha cluture





Friday, October 28, 2011

Balozi Seif aenda Marakani

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi anaondoka Nchini leo kwa safari ya Kikazi ya siku kumi Nchini Marekani.
Balozi Seif aliyepata mualiko kutoka kwa shirika la uwekezaji vitega uchumi Afrika la Nchini Marekani anauongoza Ujumbe wa Viongozi Sita wa Kiserikali akiwemo Mkewe Mama Asha Suleiman Iddi.
Ziara ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif inalenga Zanzibar kujitangaza zaidi Nchini Marekani katika Uwekezaji kwenye maeneo yaliyomo ndani ya Sekta za Utalii, Biashara, Elimu, Kilimo, Afya, Miundo Mbinu pamoja na Mazingira.
Viongozi anaofuatana nao katika Ziara hiyo ni pamoja na Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Fedha ,Uchumi na Mipango ya Maendeleo Mh. Omar Yussuf Mzee, Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mh. Fatma Alhabib Fereji na Naibu Waziri wa Afya Dr. Sira Ubwa Mamboya.
Wengine ni Mwakilishi wa Jimbo la Magomeni Mh. Salmin Awadh Salmin, Katibu Mkuu Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko Nd. Julian Raphael, Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwekezaji Vitega Uchumi Zanzibar { ZIPA } Nd. Salum Khamis Nassor wakiwemo pia baadhi ya Wafanya biashara.
Balozi Seif na Ujumbe wake ataanza Ziara yake kwa kukutana na Uongozi wa Taasisi ya Biashara na Maendeleo { USTDA } pamoja na Mwakilishi wa Taasisi ya Biashara na Vitega Uchumi inayosimamia Sera ya Biashara { USTR }.
Pia atakutana na Uongozi wa Shirika la Uwekezaji Vitega Uchumi { OPIG } linalofadhili Miradi ya Biashara ambapo siku inayofuata atakaguwa Bandari ya kwanza kwa upokeaji kwa wingi Bidhaa kutoka nje ya Maarekani ya Houston kwenye Ghuba ya Mexico pamoja na kukutana na Washirika wa masuala ya Biashara Mjini Houston.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif na Ujumbe wake ataendelea na ziara yake katika Mji wa Florida kwa kukitembelea Chuo Kikuu cha Kilimo na Ufundi cha Florida { FAMU }. Balozi Seif anatarajiwa kuondoka Washington Nchini Marekani Tarehe 6 Novemba 2011 na kurejea nyumbani akiuacha Ujumbe wake kuendelea na ziara ya siku tatu ya kukutana na Viongozi wa Taasisi mbali mbali za Uwekezaji Nchini humo ukiwemo Uongozi wa Benki Mashuhuri Duniani ya Exim Bank.
Othman Khamis Ame

Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Mafundi wa shirika la Umeme Zanzibar wakiwa katika matengezo ya taa za barabarani katika eneo la Mnazi Mmoja karibu na Bawaza la Wawakilishi wa Zamani



Thursday, October 27, 2011

Balozi wa Finland akutana na Balozi Seif Ali Iddi afisini kwake Vuga-Zanzibar

BALOZI WA FINLAND NCHINI TANZANIA BIBI SINIKKA ANTILA AKIZUNGUMZA NA MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDDI

Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi apokea hundi ya shilingi milioni khamsini

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDDI AKIPOKEA HUNDI YA SHILINGI 50,000,000/- KUTOKA KWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO MH. LEONIDAS GAMA KUCHANGIA MFUKO WA MAAFA Z’BAR

Tuesday, September 27, 2011

Marehemu Abdulrahman Babu

Marehemu Babu alikuwa jemedari wa mapinduzi ya Zanzibar

Wednesday, September 21, 2011

Muktasari wa Sensei Rumadha Fundi ”Romi”(Sandan)



Rumadha Fundi, “Sensei Romi”Mvuto wangu katika sanaa ya Karate ulianza wakati nilikuwa mdogo mnamo miaka '70s pale Kariakoo,jiji Dar, lakini asili ya kwetu ni Tabora. Kwa bahati nzuri, jirani yetu pale mtaani(Aggrey/Congo) Dar-es-salaam ambako Sensei Bomani alikuwa anakuja kuwafuata baadhi ya wanafunzi wake enzi hizo. Hapo ndio ulikuwa mwanzo wangu wa kujua hasa kuhusu Goju Ryu Karate.
Mwaka '78 mwishoni nilipata fursa ya kutembelea “Hekalu la Kujilinda” Zanaki Dojo Kan Shibu, nakuongea na Senpai Magoma Nyamuko Sarya. Kipindi hicho Sensei Bomani alikuwa amekuja toka Marekani na kuja kuwafanyia mitihani wa daraja la “Nidan”kina Senpai Magoma Nyamuko Sarya (Mwafunzi kiongozi), Senpai Tola Sodoinde Malunga, Sensei Gamanya nk. Ndipo nilipoanza shughuli za mafunzo kama”Teenager class”lilijulikana kama (Bomani Brigade)
Baada ya mtiani wa mkanda wa kahawia '81, kiongozi wetu (Senpai Magoma) aliondoka kwenda India na Phillippines kusomea sanaa mbalimbali na Yoga , ndipo na mimi nikajiunga nae huko India na baadae kwenda Sweden mnamo mwaka wa '85 katika shule ya Yoga”Internation school of Intution Practice” au katika lugha ya Sanskrit ambayo ndio inatumiwa na Yoga hujulikana kama “Prakshimata - Ananda Nilayam” huko, Gullringen, Vimmerby, Sweden.
Hapo ndipo lipohitimu ualimu wa Yoga baada ya kozi ya miaka miwili na kurudi tena Calcutta, India kwa Master mkuu wa Yoga duniani na hatimae kupata ngazi ya juu katika mafunzo ya Yoga mnamo mwaka wa '90 “Avadhuta”.
Vile vile nilipata fursa ya kwenda Houston, Texas mwaka '88 na kuendelea na mafunzo ya Karate mtindo wa “Okinawa Goju Ryu” chini ya uongozi wa Master Sensei Morio Higaona mwenye Dan 10, kiongozi mkuu wa “International Okinawan Goju Ryu Karate -Do Federation” na kupata fursa ya kupata daraja la kwanza '89 toka kwa Master Higaona huko Tampico, Mexico chini ya uongozi wa Sensei Mario Falcone wa Mexico na Sensei Ramon Veras wa Houston, Texas. Hawa ni moja ya walimu walio nisaidia kwa dhati katika sanaa ya Karate. Ninapenda kutowa shukran nyingi kwa walimu wote ambao waliweza kunifundisha sanaa hii sehemu zote zile nilizoweza kushiriki katika fani hii kama vile, Master Morio Higaona, Master Teruo Chinen, Sensei kiongozi wa Okinawa Goju Ryu, in Okinawa, Sensei Matsuda, na Sensei Muramatsu.Hao wote ni viongozi wa ngazi za juu sana duania katika sanaa ya mtindo wa Goju.
Kwa sasa hivi nina daraja la tatu “Sandan”mkanda mweusi kwa muda mrefu sasa. Kumbu kumbu yangu kubwa ni kuwa na ushirikiano mwema na wanafunzi wengi wa zamani pale “Hekalu la Kujilinda” ambao sasa hivi bado wapo mbele katika kusaidia vijana kama Sensei Maulid Pambwe, Rashid Almas, Mohamed Murudker, Wilfred Melkia, Geofrey Sawayael “Shoo”, Mbezi, Metthew huko Mwanza, Ndaukile,Edgar Kaliboti huko Sidney Australia, Salum Kitwana Khamisi huko UK. Hata wale wote ambao nimewasahau popote pale duniani.
Pia, natoa shukran nyingi sana kwa mtu muhimu sana katika maisha yangu ya kisaa ya Karate na Yoga ambaye ulikuwa ndio mashine ya mafanikio yangu ngazi zote hizo, Senpai Magoma Nyamuko Sarya(Mahadev/Mrnal) popote pale alipo nasema,”Shkran”.
Mipango ya uendelezaji sanaa hii kwa miaka ya mbele huko Tanzania ni muhimu sana. Moja ya hiyo mipango ni siku moja kufungua chuo cha sanaa ya kujilinda na kutumia nyezo za Karate”Kobudo” Kama vile “Sai, Tonfa, Nunchaku,Bo, Shuri, “Three section Nunchaku” nk. Kwa ajili ya kufundisha Tanzania. Ingawa sio leo wala kesho, bali ni moja ya mipango ya mbele huko katika maisha nitaporudi Tanzania, nakuwashirikisha walimu wengine wenye uzoefu mwingi katika kutumia nyenzo hizo.

PRESS RELEASE

Uongozi wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya migodi Afrika { AFRICA BARICK GOLD } inakusudia kuandaa ampango wa kusaidia vifaa vya uokozi kwa vyombo vya usafiri wa baharini kwa lengo la kupunguza maafa wakati zinapotokea ajali baharini.
Mjumbe wa Bodi hiyo Balozi Bakari Mwapachu ametoa kauli hiyo wakati akiwasilisha salamu za rambi rambi kwa mweyekiti wa Kamati ya Taifa ya Maafa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo Afisini kwake Vuga Mjini Zanzibar. Balozi bakari Mwapachu amesema utafiti unaonyesha kwamba vyombo vingi vya usafiri wa baharini haviwezi kutosheleza vifaa vya uokozi wakati vinapopatwa na ajali.
Amesem Uongozi wa Bodi hiyo utaandaa utaratibu wa kuzungumza na Taasisi na Mamlaka zinazosimamia usafiri wa baharini ili kuona mpango huo unaanza kutekelezwa ambapo utahusisha pia na vyombo vidogo vidogo vya uvuvi.
Balozi Mwapachu ameiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kujenga Hoja kwa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiuchumi ya Afrika Mashariki kwa kuishauri iangalie mazingira ya kujenga kituo cha Mawasiliano Hapa Zanzibar. Bodi hiyo imetowa mkono wa pole kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuchangia shilingi Milioni 60,000,000/-,
Taasisi nyengine zilizochangia mfuko wa maafa ni kampuni ya Elewana Afrika inayoendesha Biashara ya Hoteli Tanzania pamoja na Uongozi wa chama cha NCCR Mageuzi .
Mweyekiti wa Chama hicho Bwana James Fransis Mbatia amesema changamoto iliyopo ni watu wote wenye mapenzi na janga hili wanaongeza ushirikiano katika kusaidia kukamilisha kutatua tatizo hili.
Akipokea michango hiyo Mwenyekiti Kamati ya Taifa ya Maafa Zanzibar Balozi Seif ameendelea kuzisukuru Taasisi na jumuiya zilizojitolea kusaidia tatizo hili la maafa ya kuzama kwa meli Zanzibar.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Wednesday, September 14, 2011

UN pays tribute to the victims of Zanzibar boat accident

The United Nations System in Tanzania observed a minute of silence on Monday this week in remembrance of the victims of the boat that capsized off the coast of Zanzibar on early morning Saturday, September10th.
At an emergency Town Hall meeting called for at the UN Compound, the United Nations Resident Coordinator Alberic Kacou told UN staff in Dar es Salaam that immediately after hearing news on the disaster, the UN provided assistance in the form of blankets, gloves, water and high-calorie biscuits for the survivors.
He also noted that all UN staff stationed in Zanzibar have been accounted for as being safe although some have lost family members and are highly traumatized by the tragedy.
“A UN counselor has been sent to Zanzibar to provide post traumatic counseling to our colleagues. She reports that the situation is very difficult,” Kacou said. The Resident Coordinator affirmed that the UN is working hand in hand with the government in dealing with the situation.
On his part, the UN Secretary-General Ban Ki- Moon has sent condolences to the Government and people of the United Republic of Tanzania and Zanzibar and the families of the victims.
The Secretary-General said he is “profoundly saddened by the tragic loss of life” and “wishes a speedy recovery to the people who survived the accident.”
“The United Nations stands together with the people of Tanzania at this tragic moment,” said the UN Secretary General.
The sunken boat christened MV Spice Islander was heading to the island of Pemba from Zanzibar when it capsized in the wee hours of Saturday morning near Nungwi Village. Many lives have been lost. Following the incident the Government announced three days of mourning during which the national flag will be flown at half mast countrywide.
At the advisory services level, the activities consisted in:
-The UNDP assisted the department of Disaster Management (DMD) to organize and coordinate the response through the UNV placed in that office.
-The WHO team joined the team of the Ministry of Health Senior officials to provide advises on the organization of the emergency management at the main hospital.
-A UNICEF team assisted the Hospital for the “Prise en charge” of the children together with Save the Children.
-The UN stress advisor and counselor undertook collective debriefings and counseling with rescue teams to anticipate on eventual Post Traumatic Stress Disorder (PTSD) syndromes, specifically with teams having dealt with women, children and dead bodies management.
On the material support, the UN provided through different UN agencies respective contribution:
Logistics - shelter
.Tents and tarpaulins (200mx1) used on the three sites
General supply & Medical
• 52 boxes of biscuits (Nungwi & Mnazi Moja)
• 500 blankets (200 Unguja & 300 Pemba)
• 1680 Bottles of water for the rescue workers and survivors
• 50 boxes of IV fluids
• 100 boxes of Canula
• 200 rolls of plaster
• 200 rolls of Cotton wool
• 10 litres of Methylated Spirit

Hizb ut-tahriri rambi rambi rambi

HIZB UT-TAHRIR AFRIKA MASHARIKI YATOA RAMBI RAMBI KWA MSIBA WA KUZAMA KWA MELI.
Hizb ut-Tahrir Afrika Mashariki imepokea kwa huzuni na masikitiko makubwa taarifa ya kuzama kwa meli ya Spice Islander iliyotokea usiku wa kuamkia leo tarehe 10/09/2011 katika eneo la mkondo wa Nungwi baina ya kisiwa cha Pemba na Unguja, na tunaungana na walioathirika kuwafariji kwa msiba huu na kuwataka wawe na subra katika kipindi hiki kigumu.
Aidha, tunatangaza kwa ulimwengu wa kiislamu kwamba una wajibu kwa haraka kusaidia katika uokozi na kuzisaidia familia zilizopotelewa na ndugu ambao ni nguvu kazi ya familia hizo.
Ajali hii ni kielelezo wazi ziada cha kushindwa kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kutoa usafiri wa uhakika baina ya kisiwa cha Unguja na Pemba pia kushindwa kwa mamlaka zake
husika kusimamia vyema usalama wa abiria na uokozi.
Wakati Hizb ut-Tahrir Afrika Mashariki tukiwafariji kwa subra na ustahamilivu wote
walioathirika, pia tunatamka wazi kwamba ni dola ya kiislamu ya Khilafah pekee ndio yenye dhamira ya kweli na ya kimaumbile katika kulinda na kuokoa maisha ya watu.
Masoud Msellem
Naibu Mwakilishi kwa Vyombo vya Habari
Hizb ut-Tahrir Afrika Mashariki

Tuesday, September 13, 2011

Mola awape Subra wafiwa wote katika kipindi hiki kigumu cha Msiba!


Na Ramadhan Himid, Zanzibar
Mengi yamesemwa na yanaendelea kusemwa juu ya msiba mkubwa uliolikumba taifa huko Zanzibar katika usiku wa kuamkia tarehe 10 Septemba mwaka huu wakati Meli ya MV Spice Islander iliyokuwa ikitokea Zanzibar kuelekea Wete Pemba kuzama katika mkondo wa Nungwi, Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Wale wenye imani inayofanana na mimi huwa kila tunapopatwa na jambo zito kama hili hulielekeza moja kwa moja kwa Mola wetu kwa kusema “Inalillah Waina iraih rajiuun”, yaani, “Sisi sote ni Waja wa Mungu na kwake yeye tu ndio Marejeo”.
Bila shaka lililoandikwa na Mungu halipanguki, na tukiamini hilo tutakubaliana pia kwamba sisi tuliwapenda sana jamaa zetu ila Mungu amewapenda zaidi, na yeye tu pekee ndiye mwenye maamuzi sahihi ya kufanya apendavyo.
Sina lengo la kukumbusha kilio matangani, lakini msiba huu ni mkubwa na umemgusa kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyengine na ndio maana tunasema ni msiba wa kitaifa ambapo nami kupitia kalamu yangu hii sinabudi kutoa rambi rambi yangu kwa ndugu zetu tuliowapoteza
Kwa hakika Zanzibar nzima ilijinamia na haikuwa rahisi mtu kujizuia hisia zake na watu walikuwa na kila sababu ya kuangua vilio vyao na hata kushindwa kula.Tunasema ni msiba mkubwa haujawahi kutokea , na tumuombe Mungu atuepushe kwa hili na jengine.Amin.
Mungu atupe subra katika kipindi hiki kigumu kwa kuwapoteza jamaa zetu 197 ambao walifariki dunia na 619 waliookolewa. Ni kipindi kigumu lakini kwa kuwa mwanadamu amepewa sahau, inshaallah Mungu atatupa lenye kheir na sisi zaidi ya hao tuliowapoteza.
Ajali hii mbali na kutukumbusha ajali ya Mv Bukoba iliyotokea Tanzania Bara, bali pia inatukumbusha kuwa ni takribani miaka miwili hivi ambapo MV Fatih ilizama chini ya Bandari Zanzibar May 27, 2009 ambapo tuliwapoteza watu saba.
Mbaya zaidi kinacholeta taharuki kwa ajali hii ya MV Spice Islander ni kwamba idadi halisi haijulikani hadi sasa kwani inasemekana meli hiyo ilisheheni pomoni kuliko uwezo wake wa kawaida huku ikiwa na tani nyingi za mizigo.
Idadi ya waliokata tiketi inasemekana ni 610 lakini hofu ni kwamba majeruhi waliopatikana ni 619 na waliopatikana wamefariki ni 197, ni sawa na 816. Lakini ukifuatilia kwa karibu watu wengi bado wanaendelea kuwatafuta jamaa zao ambao walikuwemo katika meli hiyo, tena wengine wakiwa na watu watano ama zaidi, hebu na tujiulize meli hiyo ilikuwa na abiria wangapi?
Hili ni swali zito ambalo kila mmoja wetu anaweza kuwa na jawabu yake mwenyewe, lakini ni vyema wenye vyombo vya usafiri wa majini pamoja na Mamlaka husika kila mmoja akatekeleza wajibu wake kwa kuweka mbele maslahi ya umma kuliko maslahi yao binafsi. Umefika wakati kuhakikisha kwamba kunakuwepo kwa usimamizi wa karibu wa kuhakikisha kila meli inakuwa na idadi maalum ya abiria na inapakia kadri ya uwezo wake, tuache tabia ya kujali kitu kuliko utu.
Ni vyema pia zikawapo kumbukumbu maalum za wasafiri jambo hili litasaidia sana kujua idadi halisi kuliko kuzusha taharuki mitaani kama ilivyo hivi sasa ambapo kila mmoja anasema vyake.Jambo hili si gumu iwapo kila mmoja atatekeleza wajibu wake ipasavyo kwa kujali uzalendo na uchungu wa nchi yake. Aidha umefika wakati kwa Mamlaka husika kutoa taaluma ya wajibu wa msafiri na haki zake akiwa safarini pamoja na wajibu wa mwenye chombo na wafanyakazi wake aliowaajiri wakiwa wao ndio hasa dhamana wa chombo hivyo wakati wa safari.
Ninalisema hili kwasababu maalum, kwanza inasemekana kuwa chombo hicho kilijaza kupita kiasi na kabla ya kuondoka bandarini hapo kilikuwa tayari kimeshalemewa upande mmoja na hadi baadhi ya waliokata tiketi kuahirisha kusafiri kwa siku hiyo, lakini kwanini wafanyakazi wa chombo hicho nao wakashindwa kutimiza wajibu wao kwa kupunguza ama mizigo au abiria badala tu ya kuruhusu kuondoka bandarini ilhali wanajuwa kuwa lolote linaweza kutokea.
Kwa upande wa abiria, naamini walijua kuwa chombo kilijaza kadri ya uwezo wao lakini nao kama binadamu huwa hawapewi haki zao kama wasafiri na hii pia inatokea hata kwa usafiri wa nchi kavu abiri wanapodai kuwa chombo kinaenda mbio hutishiwa kuteremshwa njiani ama ndio dereva akakasirika na kuondeza mwendo zaidi.Ndio maana nikasema taaluma hii izidi kutolewa kuelezea haki na wajibu wa msafiri na msafirishaji wakati wa safari.
Tukishindwa kuyafanya haya kwa kuamini tu kuwa mwenye sukani ndiyo mwenye uamuzi wa kufanya atakavyo, tunaweza tukaharibikiwa mno, lakini kama tutakuwa na utaratibu maalum wa kuwajibishana kati ya mwenye chombo kuhakikisha kuwa chombo chake kinakuwa kizima, dereva (kapteni, rubani, baharia) anajali maisha ya aliowapakia na abiria kujua haki zake kutonyamazia kasoro ambazo zinaweza kupoteza uhai wake ….hapo tutakuwa salama!
Waswahili wanasema “ukupigao ndio ukufunzao”,ni wakati mwafaka hivi sasa kuwa na vyombo vya kisasa vya usafiri pamoja na kuokolea pindipo kutatokea maafa makubwa kama haya,Mungu atuepushie.
Serikali yetu nayo lazima iweke kipaumbele cha pekee kwa kuhakikisha kwamba tunakuwa na vyombo vya kisasa vya usafiri wa majini, kwani wengi wetu tunategemea usafiri wa bahari ambao ndio nafuu kuliko usafiri wa anga kwa safari za kwenda Pemba na Dare-es-Salaam , hasa ikizingatiwa kuwa hakuna usafiri mwengine mbadala kutokana na visiwa vyetu kuzungukwa na bahari.
Kwa kweli taifa limepoteza rasilimali muhimu sana kwa uzembe tu wa watu fulani ,inasikitisha na inauma sana kuona watu wengi wamefariki katika ajali hiyo , hasa wakiwemo wanawake na watoto.
Tuiachie Tume ya Usalama wa Taifa fanye kazi yake, lakini haki lazima itendeke na kusiwepo upendeleo kwa kuwafumbia macho baadhi ya watu ambao tukiendelea kuwafumbia macho kuna siku watatufumbua macho huku tumekufa.

Taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu maiti zilizookotwa Mombasa

PRESS RELEASE
Maiti tano zinazofikiriwa kuwemo kwenye meli ya m.v spice zimeokotwa katika ufukwe wa mombasa nchini Kenya. Mwenyekiti wa kamati ya taifa ya maafa zanzibar Makamu wa pili wa rais wa Zanzibar Balozi seif ali iddi ameeleza hayo afisini kwake vuga wakati akiendelea kupokea salamu za pole kutoka kwa wawakilishi wa taasisi na jumuiya mbali mbali waliofika fasini hapo kuwafariji.
Balozi seif amesema taarifa hizo zimekuja kufuatia mawasiliano kati ya serikali na Afisi ya ubalozi mdogo wa Tanzania uliopo mombasa nchini Kenya. Amesema maiti hizo tano zinafanya idadi ya maiti waliopatikana hadi sasa kufikia 202.
Makamu wa pili wa rais amezishukuru taasisi zote zilizotoa mchango wao ambao unaashiriia kukugwa na msiba huo.
Taasisi zilizowasilisha ubani wao ni pamoja na chama cha mapinduzi CCM makao makuu,wabunge wanawake wa bunge la afrika mashariki,jumuiya ya khoja shia isnashir ya afrika, uongozi wa baraza la wawakilishi Zanzibar,arusha wazee club, benki ya NMB kwa kusirikiana na baraza la manispaa Zanzibar pamoja na benki ya vitega uchumi Tanzania { TIB } pamoja na Kampuni ya IPP Media ya Dar es Salaam.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohd Aboud Mohd amepokea michango kutoka taasisi tofauti zilizohamasika kuchangia familia zilizopatwa na maafa hayo.Waliochangia fimilia hizo ni pamoja na jumuiya ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi Zanzibar{ zapha + }, Taasisi ya uwekezaji vitega uchumi Zanzibar { ZIPA }, Jumuiya ya Wanasheria Zanzibar
{ Zanzibar law Society }, Taasisi ya Huduma za Viwanja vya Ndege Tanzania { ceo }.
Akitoa shukrani zake Waziri Aboud amesema kwamba nia ya Serikali ni kuona kuendelea kuwatafuta watu wote ambao bado hawajapatikana kufuatia ajali hiyo.
Wakitoa salamu zao za pole wawakilishi wa Taasisi hizo wameipongeza Serikali kwa jitihada zake za kuleta Heshima ya nchi kutokana na kukabiliana vyema na maafa hayo kwa Ushirikiano wao wa karibu na Wananchi na Taasisi za Uokozi. Jumla ya shilingi la Kitanzania milioni148,200,000/- zimepokelewa kutoka kwa Taasisi na Jumuiya tofauti za ndani na nje ya nchi.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Monday, September 12, 2011

September 11,2011

Statement attributable to the Spokesperson for the UN Secretary-General on the Zanzibar, Tanzania ferry disaster.

The Secretary-General is profoundly saddened by the tragic loss of life after a ferry capsized off the coast of Zanzibar, United Republic of Tanzania, on 10 September.

He expresses his condolences to the Government and people of the United Republic of Tanzania and Zanzibar and the families of the victims. He also wishes a speedy recovery to the people who survived the accident.

The United Nations stands together with the people of Tanzania at this tragic moment.

Sunday, September 11, 2011

Method Kilaini ndani ya KCP

MKUTANO MKUU WA KAGERA PRESS CLUB (KPC) Septemba 10, 20
PONGEZI
Kwanza ya yote napenda kuwashukuru kwa heshima ya kunialika niwe mgeni rasmi katika mkutano wenu huu mkuu. Waandishi wa habari ni sehemu muhimu katika jamii na mhimili wa nne wa jamii. Hivyo napenda kuwapongeza kwamba mliamua kuunda chombo kinachowaunganisha katika kutimiza majukumu yenu makubwa ya kuunda jumuiya na jamii ya watu kwa kuwapa habari, kuwaelimisha, kuwahamasisha na kuwapa changamoto. Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Kwa watu wa habari ni rahisi kujikuta wanararuana na kuharibiana kazi badala ya kuungana katika kutoa mema kwa watu bila kukwaza ukweli.
UMUHIMU WA WAADISHI WA HABA
1. Waandishi wa habari na vyombo vyao wana uwezo wa kujenga au kuharibu kwa sababu ndio wnaotoa habari za matukio na watu wanawaamini sana. Tajiri mmoja mmiliki wa gazeti alishindwa kumwaminisha mfanyakazi wake juu ya habari Fulani lakini alipoiweka katika gazeti lake mfanyakazi huyo alikuwa wa kwanza kmumwambia kumbe ni kweli kwa sababu ameviona gazetini. Kuposha habari huleta madhara makubwa kwa jamii.
2. Waandishi wa habari wana uwezo wa kuchokoza hata viongozi wa serikali na kuwafanya watimize wajibu wao. Mnakumbuka sakata la magogo ya miti kutoka Rufiji yaliyosafirishwa kwa wingi hata misitu ikaanza kutoweka, vilikuwa vyombo vya habari vilivyopuliza filimbi na hatua zikachululiwa. Huu ni mfano mmoja kati ya matukio mengi.
3. Vyombo vya habari vinatoa mwanya kwa watu kutoa maoni yao na kufanya sauti ya watu hata wale wanyonge isikike. Sauti ya wasio na sauti.
MAADILI YA WAANDISHI WA HABARI
Inafurahisha kuona kwamba KPC ni wanachama hai na wenye uhusiano mzuri na Baraza la Habari Tanzania (MCT). Baraza hili lina kazi siyo tu ya kutetea uhuru wa habari kufuatana na ibara ya 18 ta katiba ya Tanzania, lakini vile vile kuhakikisha wanahabari wanafuata maadili ya kazi yao. Ili kukuza heshima ya fani yenu hapa Kagera inabidi muwe wanachama hai kwa matendo katika baraza hilo. Uandishi wa habari bila maadili ni sumu kwa jamii. Mifano mikubwa ni jinsi vyombo vya habari vilivyotumiwa Rwanda na Kenya wakati wa machafuko na mauaji.
Jukumu la mwanahabari ni kutoa ukweli hata ule mchungu kwa ajili ya kujenga na kutibu jamii, kuleta uelewano na siyo chuki, mshikamano na siyo utengano, kujenga na siyo kubomoa. Hiyo kazi mtaifanya kama mtasaidiana kufuatana na maadili yanayotolewa na baraza hilo ambalo ni la hiari, huru na lisilo la kiserikali lililoanzishwa mwaka 1997, likiwa na lengo la kujirekebisha lenyewe ili lisitoe mwanya na sababu kwa wengine ikiwemo serikali kuwabana kwa kisingizio cha utovu wa nidhamu. Muwe na uwezo wa kukosoana na kuambizana ukweli.
UHITAJI WA WANAHABARI MKOANI KAGERA
Mkoa wa Kagera una uhitaji wa kupata wanahabari wengi na makini. Kuna watu wengi nje ya mkoa hasa wanakagera amabao wana kui kikubwa kupata habari za Kagera. Hivyo lengo lenu la kuitangaza ni zuri na lenye tija kwa sisi sote. KPC ina kazi kubwa na nzuri ya kuwasaidia na kuwahamasisha wanahabari wa mkoa wa Kagera kutimiza majukumu yao ya:
a. Kutangaza mambo mengi mazuri yanayofanywa Kagera kwa wanakagera na ulimwengu mzima. Ni ninyi mtaweka Kagera kwenye ramani ili mtu asiulize Kagera ni nini? Mnategemewa kuienzi na kuiuza Kagera, utajiri wa kitalii, mazao yake mazuri, utamaduni wake na mafanikio yake. Ninyi muwe wa kwanza kujifunza na kujua Kagera na utajili wake. Tembeleeni sehemu mbali mbali na kutaneni na watu mbali mbali.
b. Kurahisisha kuomba misaada kwa ajili ya Kagera wakati wa shida na maafa kwa kuyatangaza. Mfano ni kimbunga kilichopiga Muleba. Ilituwia rahisi kuomba misaada nje kwa sababu taarifa ilitoka kwenye vyombo vya habari na hatukupashwa kutoa maelezo mengi. Hivyo juzi nilikwenda huko kugawa mabati na mashuka kutoka Caritas Tanzania kwa niaba ya kanisa Katoliki, ninawashukuru sana.
c. Kusisimua viongozi mara nyingine kutoka usingizini kwa kuyaainisha matatizo ambayo hawajayafanyia kazi. Kazi yenu siyo kila mara kufuatana nyuma ya viongozi na kuripoti majigambo yao na kuwafurahisha, nendeni na kule amabako wamesahau na kuonyesha uozo uliopo. Msiogope, mwandishi wa habari anayeogopa na kuwa kibaraka mradi kula hatakuwa hata siku moja mwandishi makini mwenye kuheshimiwa. Fichueni uozo, uzembe na hata ufisadi kama upo hapa Kagera na hapo vitafanyiwa kazi.
d. KPC iwe shule kwa ajili ya waandishi wadogo ambao bado hawajapata elimu kubwa ya uandishi ili waweze kuleta habari kutoka vijijini. Nashukuru na hongera nma uhusiano mzuri na (MCT) na Mfuko wa Habari Tanzania (TMF) na mmefanya kwa mafaniko mradi mkubwa nao, na wao wako tayari kuendelea nanyi. Hivyo hakikisha wale mtakaowachagua wawe na uwezao wa kuendeleza juhudi hizo.
e. Chama kitoe msaada kwa magazeti na vyombo vya habari vya hapa mkoani Kagera na kuanzisha vingine. Najua wengi kula yao ni magazeti na vyombo vya habari vya jijini Dar es Salaam na Mwanza na sina ugomvi nal kwa sababu na linatusaidia kupeleka habari na maoni yetu taifani. Lakini ujuzi wenu usaidie vile vile vyombo vya matumizi ya ndani ili Bukoba/Kagera iwe kituo cha habari (hub).
f. Vyombo vyetu vya habari viwe uwanja wa wanachi kuleta maoni, mawazo, furaha, manunguniko na mafaniko yao kwa umma. Nafurahi sana kusikiliza redio zetu.
g. Changamoto moja ni kwamba waandishi wa habari wengi wako hapa Bukoba mjini na wilaya nyingine hazina hata mmoja. Nilikuwa Muleba Mkuu wa wilaya akaniambia kule hakuna mwandishi hata mmoja, nikashangaa. Najua ninyi hamtahamia Muleba lakini mnaweza kuwahamasisha wana Muleba walu wachache wakajihusisha na uandishi wa habari hata kama siyo wataalamu wakubwa nanyi mkahariri habari hizo. Vile vile haitoshu ninyi kuandika habari za Dar es salaam tu na labda kidogo za Bukoba mjini hasa wanapotembelea viongozi wa juu bali fanya utafiti juu ya sehemu zote za Kagera.
WANAHABARI KAMA FAMILIA MOJA
Inajulikana kwamba magazeti na vyombo vya habari vina wenyewe na kila mwenye chombo ana lengo lake. Mwandishi au mtangazaji lazima afuate sera ya mwenye chombo na vingine vinapingana katika mielekeo yao. Kwetu hilo siyo baya kwa sababu linatupa sisi wadau mitazamo tofauti ili nasi tuweze pupambanua kati ya pumba na mchele. Licha ya hilo ninyi wanahabari mnapashwa kuwa marafiki na ndugu bila uhasama ingawa mara nyingine mnapingana katika maandishi yenu mradi usiseme uongo bali iwe tu ni mitazamo na mkazo tofauti katika ukweli huo huo.
Mkiwa familia moja hapo mipango yenu ya maendeleo itafanikiwa. Leo uko gazeti/radio/TV ya mlengo wa kulia, kesho utakuwa na lile la mlengo wa kushoto bali wewe ubaki mwanahabari. Pawepo uwezekano wa kuketi na kuchambua pamoja habari ndani na nje ya vyombo vya habari ili kupanua ugo wenu. Kuwa na miradi ya pamoja kama vyombo vya habari, mini press na hata SACCOS ya kujikimu. Mwanahabari mwenye njaa husaliti fani yake kwa sababu hulipwa kupindisha habari ambacho ni mwiko na aibu kwa manahabari na madhara yake ni makubwa kwake binafsi na kwa jamii.
Ni vizuri sana kwamba mnaweka mazingira kwa wale wadogo kufanya kazi kama kuwapa kamera, scanner, computer, printer vya kuandikia stori zao na mengine. Kupitia hapo watajifunza na kukua kuwa wanahabari wanaojitegemea.
Uanachama siyo tu kupata faida lakini vile vile una majukumu yake. Mafanikio hutokana na jasho na juhudi. Ukiwa mwanachama kwa mfano itabidi ulipe ada yako mapema ili chama kimudu kazi zake, ushiriki katika mikutano inapoitwa, uchangie kwa namna mbali mbali kwa hali na mali. Asiyetupa haokoti, tupa kwanza na hapo utaokota mengi. Uwajibike, mkipata mradi wa kutekeleza, usaide kuutekeleza vizuri na kutoa ripoti zote zinazohitajika kwa wakati ili waweze kuwaamini na kuwapa miradi mingine. Usiganganie marupurupu ya miradi bila kuitolea jasho lako. Asiyefanya kazi asile.
UCHAGUZI
Mimi simpigii ye yote kampeni na wala sijui nani anagombea, ila nawaombea uchaguzi wenye tija na uwaweke viongozi waostahili na wenye sifa katika safu za kutoa maamuzi. Wawe viongozi wabunifu wataoimarisha siyo tu vilivyopo bali watabuni na njia nyingine za kukiendeleza chama na fani ya uandishi Kagera kwa ujumla. Wawe viogozi wawajibikaji na waaminifu wataoaminiwa siyo tu nanyi lakini hasa wafadhili wa nje ili misaada inayotolewa ifikie lengo lake kwa wakati na kwa mafanikio. Viongozi wa heshima na ustaarabu ambao wataheshimiwa na wote hata viongozi wa serikali na taasisi nyingine ili wawe na uwezo wa kuwasilana nao bila shida. Viongozi wenye kujali kiasi kwamba wataweza kuwasiaidia vijana wanaotaka kuingia fani hii lakini hawajui waanzie wapi au wameingia lakini bado wanyonge bila kuwadhalilisha, kuwakandamiza au kuwaomba hongo.
Ndugu mwenyekiti napenda kumalizia kwa kuwatakia kila la heri na fanaka katika mkutano wenu mkuu ambao utatoa vingongozi bora wa kusimamia fani hii muhimu katika kipindi kijach cha miaka mitatu hapa Kagera. Sisi tuko pamoja nanyi.
Mwenyezi Mungu awabariki
+Method Kilaini
Askofu Msaidizi
Jimbo Katoliki la Bukoba

Sunday, September 4, 2011

Taarifa kwa vyombo vya habari

PRESS RELEASE
Ujenzi wa Afisi za Wabunge ndani ya Majimbo ni uamuzi sahihi wa Bunge La Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha huduma za Wananchi zinapatikana kwa haraka muda wote. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Kitope amesema hayo katika hafla fupi ya kukabidhiwa Afisi ya Jimbo hilo baada ya kukamilika Ujenzi wake.
Hati za Makabidhiano ya Afisi hiyo ya Mbunge wa Kitope imetiwa saini kati ya mbunge huyo Balozi Seif na Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B Nd. Vuai Ali Vuai ambapo ujenzi wa Afisi za Wabunge unasimamia na Afisi za Wakuu wa Wilaya. Akikabidhi hati hiyo Mkuu wa Wilaya ya Kakaskazini B Nd. Vuai Ali Vuai amesema ujenzi huo unafuatia azimio la bunge la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania wa kujenga Afisi za Wabunge Majimboni.
Akipokea Afisi hiyo mbunge wa jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi amewahakikishia wananchi hao kwamba yeye na mwakilishi wa Jimbo hilo Mh. Makame Mshimba wataendelea kushirikiana na Wananchi hao ili Maendeleo ya haraka ndani ya Jimbo hilo yafikiwe. Wakati huo huo Balozi Seif Ali Iddi ameutembelea ushirika wa mwendo wa jongoo wa Kazole ambao unajishughulisha na ukulima wa mboga mboga.
Akiunga mkono juhudi za wanaushirika hao Balozi Seif Amekabidhi ndondo kwa kuendeleza ujenzi wa Afisi ya Tawi la CCM la Kijiji hicho pamoja na mpira wa Maji na vifaa vyake na kuahidi kutoa makalbi ya kisima ili kuwaondoshea shida ya upatikanaji wa maji katika mradi wao wa kilimo.
Balozi Seif pia amekabidhi msaada wa Matofali, Saruji, mchanga na fedha za fundi kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Tawi la CCM La Kichungwani na kushauri ni vyema Tawi hilo likaanza kutoa huduma mwaka ujao. Vifaa na msaada huo kwa Kikundi cha Ushirika cha Uwendo wa Jongoo na Afisi za CCM vimegharimu Shilingi Milioni Moja Nukta Moja.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Thursday, September 1, 2011