Wednesday, February 22, 2012

Mkuu wa Wilaya awataka watendaji wa wilaya ya mkoani kushirirki ipasavyo katika kamapeni ya chanjo ya Surua

Na Is-haka Omar ZPC Zanzibar
Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Bw. Jabu khamis Mbwana amewataka watendaji wa Wilaya za Mkoani Pemba kushirikiana ipasavyo katika kukabiliana na ugonjwa wa surua .
Mkuu huyo wa wilaya ya mkoani amesema viongozi wa afya ,masheha wa shehia nane za wilaya hiyo, madiwani na viongozi wa vyama wanapaswa kushirikiana pamoja katika kulikabili tatizo la ugonjwa wa surua katika shehia hizo.
Ndugu Mbwana ametoa wito huo huko ukumbi wa Umoja ni Nguvu wakati akizungumza na viongozi na walimu wakuu wa skuli saba za shehia hizo ambazo zinakabiliwa na mripuko wa maradhi ya surua katika shehiya hizo.Shehia za Mizingani,Mgagadu,Ngwachani,KisiwaPanza,Chokocho,stahabu,wambaa, na shumbageni zinaelezwa kukumbwa na mripuko mkubwa ugonjwa wa surua katika kisiwa cha Pemba. Ndugu Mbwana amefahamisha kuwa jambo lililopelekea kutokea kwa mripuko wa maradhi hayo ni wananchi wakati wa chanjo iliyopita kudharau kuwapeleka watoto kupatiwa chanjo licha ya elimu kutolewa kabla ya chanjo hiyo.
Pamoja na hayo amesema kutokana na tatizo hilo wizara ya afya kwa kushirikiana na serikali ya wilaya ya mkoani inakusudia kutoa chanjo hiyo.

No comments:

Post a Comment