Monday, November 28, 2011

Kombe la Mapinduzi Zanzibar

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema Mpango wa kuandaa Kombe la Mapinduzi Cup umelenga kukuza Michezo pamoja na kuimarisha Ujirani mwema ndani ya Mipaka ya Afrika Mashariki.
Balozi Seif ametoa kauli hiyo wakati akizindua Kamati ya Mapinduzi Cup yenye wajumbe kumi ikiongozwa na mwenyekiti wake Mohd Raza Hassan katika Ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Mjini Zanzibar.
Alisema mpango huu unaweza kuongeza kiwango cha Michezo ndani ya kanda hii endapo Wapenda michezo na wadau wote wataonyesha ushirikiano wao kwa kamati hii.
Balozi Seif alisisitiza kwamba Serikali haina budi kuiunga mkono Kamati hii ili kuona inafanikisha malengo iliyopangiwa.
“ Na hili nitahakikisha litatekelezwa kwa upande wa Serikali Mimi mwenyewe nitalisimamia kwa vile ndie Mtendaji Mkuu wa Serikali ”.
Alisisitiza Balozi Seif.
Aliipongeza Kamati hii kwa kuwa na wajumbe mahiri na ana matumaini ya kufanikiwa na Kamati hiyo na kuvuka kiwango cha ufanisi cha mwaka uliopita.
Akimkaribisha Balozi Seif Waziri wa Hahabi ,utamaduni, Utalii na Michezo Abdillahi Jihadi Hassan amesema Wizara ina matuimaini makubwa na Kamati hiyo kwa vile imeundwa kwa kuzingatia uwezo na uzoefu walionao.
Mapema Mwenyekiti wa Kamati ya Mapinduzi Cup Mohd Raza ameahidi kwamba Kamati yake itahakikisha inatekeleza vyema majukumu yake kwa mujibu wa matakwa ya wadau wa Michezo.
Raza alisema Kamati yao itaendelea kuzingatia zaidi huduma na burdani kwa wananchi katika mashindano ya michezo ya Mapinduzi Cup yatakayojumisha Pia Mpira wa Wavu { Netball } kwa kuzhishirikisha baadhi ya Timu za Tanzania na timu alikwa kutoka nje ya Afrika Mashariki.
Kamati hiyo iliyoundwa chini ya uwenyekiti wa Mohd Raza ina wajumbe kumi ambao ni Sherry Khamis, Ibrahim Makungu, Mwakilishi wa Jimbo la Rahaleo Nassor Jazira, Katibu Mkuu Wizara ya Habari utamaduni na Mchezo Ali Mwinyikai na Naibu wake Issa Mlingoti.
Wengine ni Ali Khalil Mirza, Taufiq Turky, Aboubakar Bagharesa pamoja na Farouk Karim ambaye ndie Mratibu wa Kamati hiyo.
Othman Khmis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

No comments:

Post a Comment