RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed
Shein ametuma salamu za pongezi kufuatia ushindi wa Rais Barack Obama wa
Marekani katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo uliofanyika hivi karibuni.
Katika
salamu zake za pongezi kwa kiongozi huyo wa Marekani ambaye
amechaguliwa kwa mara nyengine tena na wananchi wa nchi hiyo kwa kipindi
cha pili, Rais Dk. Shein alieleza jinsi alivyopokea kwa furaha ushindi
huo pamoja na wananchi wote wa Zanzibar.
Salamu
hizo za pongezi zilieleza kuwa kwa niaba yake binafsi pamoja na
wananchi wa Zanzibar anatuma salamu za pongezi kwa Rais Obama kwa
ushindi mkubwa alioupata katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni
nchini humo.
Aidha, salamu hizo zilieleza kuwa wananchi
wa Marekani wameona umuhimu wa kumuunga mkono Rais Obama na kumrejesha
tena madarakani kwa lengo la kuliendeleza na kuliongoza taifa hilo kubwa
duniani kwa kipindi cha miaka mine ijayo.
Pamoja
na hayo, salamu hizo zilieleza kuwa wananchi wa Zanzibar wanaungana na
rafiki zao wa Marekani katika kusherehekea ushindi huo uliotokana na
uchaguzi mkuu wa hivi karibuni wa Marekani ambao umempa ushindi Rais
Obama.
Dk.
Shein alimtakia uongozi mwema Rais Obama na kutoa salamu za pongezi kwa
familia ya Rais Obama akiwemo Mkewe Mama Michelle Obama na watoto wake wote Malia na Sasha Obama pamoja na wananchi wa Marekani ambao wameonesha wazi imani na uaminifu mkubwa walionao katika uongozi wa Rais Obama.
Sambamba na hayo, salamu hizo zilieleza kuwa uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya Zanzibar na Marekani utazidi kuimarika.
No comments:
Post a Comment