Tuesday, September 11, 2012

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


KUUAWA KWA MWENYEKITI WA KLABU YA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA IRINGA (IPC) DAUDI MWANGOSI 
 Zanzibar Press Club imepokea kwa masikitiko na hudhuni  taarifa ya kifo cha mwandishi wa habari wa kituo cha Channel Ten ambaye pia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari wa Iringa.  
Zanzibar Press Club inaungana na waandishi wa habari wote nchini ambao leo hii wanatekeleza azimio la jukwaa la Wahariri la kufanya maandamo ya kimya kimya, kote nchini, kwa lengo la kupinga mauwaji ya aliyekuwa Mwenyekiti Klabu ya waandishi wa habari wa Iringa, Mrehemu Daudi Mwangosi.
Katika kutekeleza azimio hilo ZPC imeamuwa kukutana na waandishi wa habari ili kuweza kueleza kusikitishwa kwao na tukio hilo lilompata mwenzetu wakati akitekeleza majukumu yake ya kila siku.
Aidha ZPC inaungana na waandishi na wafanyakazi katika tasnia ya habari nchini, Umoja wa Waandishi wa Habari nchini (UTPC), Klabu za waandishi kote nchini, MISA-TAN, MCT, JUKWAA LA WAHARIRI  n.k  pamoja na familia ya marehemu Daudi Mwangosi kwenye kipindi  hiki kigumu cha msiba, ambapo hakuna shaka kwamba tasnia ya habari nchini imelazimika kuingia matatani kutokana na matumizi mabaya ya nguvu na  mabavu ya Jeshi la Polisi.
ZPC inalaani kwa nguvu zote mauwaji hayo na yaliyofanywa na watendaji wa taasisi ya umma pamoja na kutumia nguvu nyingi kupiti kiasi zilizopelekea kifo cha mwandishi huyo.
Jeshi la Polisi limekuwa likiendeleza tabia yake ya  matumizi ya nguvu kupita kiasi kwa raia wa taifa hili. Ipo haya ya kutaka kujuwa ni hadi lini jeshi la polisi wataweza kuimarisha vyema shughuli za ulinzi bila ya kuchukuwa uhai wa mtu?
Hapana shaka yoyote kwamba kifo cha Daudi Mwangosi kimegubikwa na utata wa kutosha kuanzi mwazo hadi mwisho wa maisha yake, na hasa ukizingatia kwamba tukio hilo la mauaji limefanyika hadharani wakati  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Nd.Michael Kamuhanda alikuwa anatambua uwepo wa Daud Mwangosi  na pia umuhimu wa habari hizo kwa taifa, na kibaya zaidi ni pale kumuona Daud akiwa anafia kwenye mikono ya jeshi la polisi kulikoni?
Ikumbukwe kwamba siku zote hata katika vita waandishi wanafanya kazi bega kwa bega na askari ili kuwajuza wananchi nini kinachotokea na kinachoendelea kwenye uwanja wa mapambano.
Kutoka na kifo hicho ZPC inaomba hatua za kisheria zichukuliwe kwa wale wote waliohusika moja kwa moja na kifo cha mwandishi huyo.
Zanzibar Press Club kwa saa ingependa kuona utekelezaji mzuri wa kisheria kwa askari wote ambao walihusika kwenye kadhia hii.
Mbali na hayo, ZPC inawaomba waandishi wa habari wote wa Zanzibar wawe makini wakati wanapotekeleza majukumu yao, kwani kutokana na tukio hili limetufanya tuone kuwa Jeshi la Polisi ni Mdau anayetutia shaka katika utekelezaji wa majukumu yetu.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi Amini.
Abdalla Juma Pandu
Kaimu Mwenyekiti
Zanzibar Press Club

No comments:

Post a Comment